IGP Sirro amesema hayo leo jijini Dar es salaam, wakati akizungumza na wamiliki wa Makampuni binafsi ya ulinzi kwenye kikao kazi cha kujadili utendaji wa makampuni hayo.
Kuhusu suala la usafirishaji wa fedha, IGP Sirro, ameelekeza baadhi ya Makampuni ya ulinzi kuacha tabia ya mazoea ya kusafirisha kiasi kikubwa cha fedha na badala yake watumie Jeshi la Polisi kwa ajili ya kuhakikisha usalama wa fedha hizo huku watakaoshindwa kufanya hivyo watachukuliwa hatua za kisheria.
No comments:
Post a Comment