A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Monday, May 18, 2020

MWANAFUNZI WA DARASA LA 6 ASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI KWA KUKUTWA NA MTAMBO WAKUPIKIA POMBE HARAMU YA GONGO


Jeshi la Polisi mkoani Rukwa, linawashikilia watu watatu akiwamo mwanafunzi wa darasa la sita kwa tuhuma za kukutwa na mtambo wa kutengenezea pombe haramu aina ya gongo, pamoja na lita 20 za pombe hiyo.

Mwanafunzi huyo mwenye umri wa miaka 19 ni wa Shule ya Msingi Katusa katika Manispaa ya Sumbawanga.

Kamanda wa Polisi mkoani Rukwa, Justine Masejo, alisema kuwa watu hao wamekamatwa kufuatia operesheni maalumu iliyoongozwa na mkuu wa upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoani Rukwa, Ralph Meela pamoja na maofisa wa polisi na askari.

Kabla ya kukamatwa kwa watuhumiwa hao, alisema Jeshi la Polisi lilipata taarifa kuwa kuna watu katika kitongoji cha Katusa Manispaa ya Sumbawanga wanafanya biashara haramu ya kuuza gongo, kitendo kinachosababisha mkusanyiko wa watu wanaokunywa pombe hiyo bila kuchukua tahadhari ya kujikinga na maambukizo ya ugonjwa wa Covid-19.

Kamanda huyo alisema baada ya taarifa hizo ndipo askari polisi wakiongozwa na Meela walivamia katika eneo hilo na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao wakiwa katika eneo la tukio, huku baadhi yao wakiwa wanakunywa pombe hiyo, akiwamo mwanafunzi huyo.

“Baada ya kuwakamata watuhumiwa hao, polisi walibaini kuwa licha ya kutenda kosa la kuuza na kunywa pombe hiyo haramu, hawakuwa wanachukua tahadhari yoyote ya kujikinga kuambukizo ya virusi vya corona kwa kuwa walikuwa katika mkusanyiko..hakuna hata aliyevaa barakoa wala hakuna maji ya kunawa mikono, pia hakuna kitakasa mikono cha aina yoyote,” alisema.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages