A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Thursday, April 16, 2020

Bunge la Umoja wa Ulaya kujadiliana kuhusu corona


Bunge la Umoja wa Ulaya linatarijiwa kukutana leo kwenye kikao maalum kujadiliana kuhusu msimamo wa pamoja katika kukabiliana na janga la virusi vya corona.

Rais wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya, Ursula von der Leyen na Rais wa Baraza la Ulaya, Charles Michel watauongoza mkutano huo utakaofanyika leo jioni.

Wabunge hao wanatarajiwa kupigia kura azimio linalotaka raia wa Umoja wa Ulaya kulindwa kwa kiasi kikubwa katika kukabiliana na janga la ugonjwa wa COVID-19, umoja huo kusaidia mifumo ya afya ya nchi wanachama na mkakati sawa katika kuchukua hatua za dharura.

 Rasimu ya azimio pia inaikosoa tabia ya nchi mbili wanachama, Hungary na Poland katika kukabiliana na mzozo wa virusi vya corona.

Wabunge wengi watahudhuria mkutano huo utakaofanyika kwa njia ya mtandao na wote watapiga kura kupitia barua pepe. Spika wa Bunge la Ulaya, David Sassoli atatangaza matokeo kesho.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages