A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Tuesday, March 17, 2020

Mwigizaji maarufu wa filamu duniani Idris Elba aambukizwa virusi vya Corona

Muigizaji maarufu wa filamu duniani Idris Elba ambaye pia amewahi kutajwa na jarida la "People Magazine kuwa mwanaume mwenye mvuto zaidi duniani amethibitika kukutwa na maambukizi ya virusi vya Corona.

Kupitia ukurusa wake wa Twitter amechapisha video fupi akiwa na mkewe akizungumza alivyopata maambukizi hayo, na maendeleo ya afua yake.

Elba amesema licha ya kwamba hakuwa na dalili za homa ya mapafu, COVID-19, lakini alipima baada ya kubaini kuwa alikuwa karibu na mtu mwenye maambukizi.

Aidha, ameweka wazi kuwa anaendelea vizuri na kwamba tayari amejitenga ili kuhakikisha hasambazi virusi hivyo kwa watu wengine.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages