A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Tuesday, March 17, 2020

Mtu wa kwanza ajitolea kufanyiwa chanjo ya virusi vya corona Marekani



Binadamu wa kwanza kufanyiwa jaribio ya chanjo ya kinga dhidi ya virusi vya corona ameanza kufanyiwa jaribio hilo nchini Marekani.



Wagonjwa wanne walidungwa sindano ya virusi katika kituo cha utafiti Kaiser Permanente mjini Seattle, Washington, limeripoti shirika la habari la Associated Press.

Chanjo hiyo haiwezi kusababisha Covid-19 lakini ina jeni la virusi ambavyo vinaweza kusababisha ugonjwa.

Wataalamu wanasema itachukua miezi mingi kujua ikiwa chanjo hii, au utafiti mwingine, utafanikiwa.

Matumizi ya kemikali ya kuua wadudu na vimelea kwa kusafisha mikono imetajwa kuwa moja ya njia ya kuepuka maambukizi ta virusi vya corona
Mtu wa kwanza kujitolea kupata dozi ya kwanza ya utafiti huo siku ya Jumatatu ni mama wa watoto wawili mwenye umri wa miaka 43 mkazi wa Seattle Washington.

"Hii ni fursa ya kufurahisha kwangu mimi kuweza kufanya kitu fulani," alisema mama huyo aliyetambuliwa kama Jennifer Haller katika mazungumzo na shirika la habari la AP.

Wanasayansi kote duniani wanaharakisha utafiti wao kujaribu kupata chanjo au tiba ya coronavirus.

Na jaribio hili la kwanza kwa binadamu,lililodhaminiwa na Taasisi ya Kitaifa ya Afya nchini Marekani, umefanyika kando ili kuangalia kile ambacho kwa kawaida kingekua kikifanyika kuhakikisha chanjo inaweza kusababisha kuchochewa kwa kinga ya mwili katika wanyama.

Lakini kampuni ya teknolojia ya masuala ya vimelea wa magonjwa ambayo ndiyo inayoendesha utafiti huo, Moderna Therapeutics, inasema kuwa chanjo imekwishakutengenezwa kwa kutumia mchakato uliojaribiwa na kupimwa.

Binadamu wa kwanza kufanyiwa jaribio ya chanjo ya kinga dhidi ya ugonjwa wa corona ameanza kufanyiwa jaribio hilo nchini Marekani

Wagonjwa wanne walidungwa sindano ya virusi katika kituo cha utafiti Kaiser Permanente mjini Seattle, Washington, limeripoti shirika la habari la Associated Press.

Chanjo hiyo haiwezi kusababisha Covid-19 lakini ina jeni la virusi ambavyo vinaweza kusababisha ugonjwa.

Wataalamu wanasema itachukua miezi mingi kujua ikiwa chanjo hii , au utafiti mwingine, utafanya.

Mtu wa kwanza kujitolea kupata dozi ya kwanza ya utafiti huo siku ya Jumatatu ni mama wa watoto wawili mwenye umri wa miaka 43 mkazi wa Seattle Washington.

"Hii ni fursa ya kufurahisha kwangu mimi kuweza kufanya kitu fulani ," alisema mama huyo aliyetambuliwa kama Jennifer Haller katika mazungumzo na shirika la habari la AP.

Wanasayansi kote duniani wanaharakisha utafiti wao kujaribu kupata chanjo au tiba ya coronavirus.

Na jaribio hili la kwanza kwa binadamu, lililodhaminiwa na Taasisi ya Kitaifa ya Afya nchini Marekani , umefanyika kando ili kuangalia kile ambacho kwa kawaida kingekua kikifanyika kuhakikisha chanjo inaweza kusababisha kuchochewa kwa kinga ya mwili katika wanyama.

Lakini kampuni ya teknolojia ya masuala ya vimelea wa magonjwa ambayo ndiyo inayoendesha utafiti huo -Moderna Therapeutics, inasema kuwa chanjo imekwishakutengenezwa kwa kutumia mchakato uliojaribiwa na kupimwa.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages