A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Thursday, December 19, 2019

NMB MASTABODA NDANI YA KISARAWE!

Mkuu wa Kitengo cha Kadi wa Benki ya NMB, Philbert Casmir, akizungumza wakati akifunga rasmi mafunzo ya matumizi ya huduma mpya ya MastaBoda kwa waendesha Bodaboda wa Wilaya ya Kisarawe na vitongoji vyake. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo na Mkuu wa Kitengo cha Biashara za Serikali wa NMB, Vicky Bishubo.
Mmoja wa waendesha Bodaboda akifungua akaunti ya NMB.
Waendesha Bodaboda katika picha ya pamoja baada ya semina iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi za Wilaya ya Kisarawe.

Kampeni ya MastaBoda inayoendeshwa na Benki ya NMB kwa ajili ya kuwaunganisha waendesha Bodaboda katika mfumo wa kibenki wa kupokea malipo kwa Mastercard QR kutoka kwa wateja wa Benki ya NMB, Benki zilizounganishwa na Mastacard QR pamoja na mitandao ya simu iliyounganishwa na huduma ya Mastercard QR sasa imevuka boda hadi Kisarawe Mkoani Pwani.

Akizindua kampeni hiyo na kufunga mafunzo ya siku sita yaliyotolewa na NMB kwa waendesha Bodaboda Wilayani humo, Mkuu wa Wilaya Jokate Mwegelo amesema kampeni hiyo imefika muda muafaka katika Wilaya yake.

Jokate amesema, kama Wilaya na Serikali wamejipanga kuipokea kampeni hiyo kwa waendesha bodaboda 150 waliyozitokeza katika mafunzo hayo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages