A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Thursday, December 19, 2019

BENKI YA NMB YAAHIDI KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUKUZA UTALII

Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara Ndogo na za Kati wa Benki ya NMB, Filbert Mponzi (kuli) akizungumza na wanachama wa Chama cha Waongoza Watalii Tanzania (TATO) chenye lengo la kuhimiza ushirikiano kati yao.
Sehemu ya wageni waalikwa.

Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara Ndogo na za Kati wa Benki ya NMB, Filbert Mponzi (kuli) akibadilishana mawazo na baadhi ya wageni Waalikwa.
Benki ya NMB imeahidi kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha inasaidia harakati za Serikali kukuza Utalii nchini, ili kuinyanyua zaidi sekta hiyo ambayo inaongoza katika kuchangia pato la taifa na kuingiza fedha nyingi za kigeni ukilinganisha na sekta nyingine.

Ahadi hiyo ilitolewa na Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara Ndogo na za Kati wa NMB, Filbert Mponzi, wakati wa Chakula cha Usiku, kilichoandaliwa na Chama cha Waongoza Watalii Tanzania (TATO) na kufadhiliwa na NMB, kikihudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Profesa Adolf Mkenda.

Katika hafla hiyo iliyofanyika jijini Arusha, Mponzi alibainisha kuwa, NMB imeshaanza kutoa mikopo ya magari kwa Waongoza Watalii ‘Tour Operators Vehicle Finance,’ lengo likiwa ni kuwawezesha waongozaji kurahisisha majukumu yao na kuvutia watalii zaidi na kukuza pato la taifa.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages