Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limethibitisha kuachana rasmi na Mkurugenzi wake wa Ufundi Ammy Ninje kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kubanwa na majukumu ya kifamilia baada ya kumaliza muda wake.
Rais wa Shirikisho hilo Wallace Karia amesema Ninje anarejea nchini Uingereza na wakati wowote kuanzia sasa watamtangaza mkurugenzi mpya pamoja na msimamizi mkuu wa benchi la ufundi la timu ya vijana U17 Serengeti Boys.
Kwa upande wake, Ninje amekiri kuwa suala la familia ndilo lililomfanya ajiondoe kwenye soka la Tanzania.
No comments:
Post a Comment