Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akizungumza wakati wa mkutano wa majumuisho kilichowakutanisha wakuu wa Wilaya, wakurugenzi, Makatibu Tawala, washauri wa miradi na wakandarasi mkutano huo umefanyika leo jijini humo.
Baadhi ya wakurugenzi waliohudhuria mkutano huo.
Baadhi ya Wakuu wa Wilaya waliohudhuria
Naibu Meya na Diwani wa Kata ya Vingunguti Omari Kumbilamoto, (kushoto), akifuatilia mkutano huo
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul
Makonda amefanya kikao cha majumuisho kilichowakutanisha wakuu wa Wilaya,
wakurugenzi, wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala, washauri wa miradi na
wakandarasi na hiyo ni kufuatia ziara iliyofanywa na RC huyo katika kukagua miradi
mbalimbali ya kimaendeleo jijini humo.
Akizungumza na watendaji hao Makonda
amewapongeza watendaji kwa juhudi wanazozifanya katika kuleta maendeleo na
kuwataka watimize ahadi zao kama walivyohaidi na hiyo hasa ni katika ujenzi wa
vituo vya afya Buguruni na Kigogo kwa kuikamilisha kwa wakati huku
akifurahishwa na kasi ya ujenzi wa hospitali za Wilaya za Ilala na Kigamboni
ambazo zinajengwa kwa jumla ya shilingi bilioni 1.5 fedha ambazo zilizotolewa
na Rais John Joseph Magufuli katika kuboresha sekta ya afya.
Aidha ameitaka Halmashauri ya Ubungo
kuongeza kasi zaidi katika utatuzi wa kero za wananchi na kuwataka viongozi
kuacha siasa na kuchapa kazi huku akielekeza nguvu zaidi iwekwe katika
shughuli za kimaendeleo.
Vilevile amewasisistiza wataalamu wa
kusimamia miradi jijini humo kushirikisha wazawa katika miradi mikubwa ya
kimaendeleo pindi tenda zinapotangazwa ili kuweza kuwainua na kuwapa fursa
zaidi.
Wakati huo huo Makonda ametumia
nafasi hiyo kuzipongeza halmashauri zote na watendaji wao kwa kuufanya Mkoa huo
kuwa kinara katika ukusanyaji wa mapato kwa kipindi cha robo mwaka kwa
kukusanya zaidi ya shilingi bilioni 118.4 ikifuatiwa na Jiji la Dodoma
lililokusanya bilioni 57.3 na Jiji la Mwanza shilingi bilioni 22.9 huku
Wilaya za Ilala na Kinondoni zikifanya vizuri zaidi nchini.
Ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es
Salaam ilimulika miradi mbalimbali ya kimaendeleo katika Wilaya zote jijini
humo na katika ufanyaji wa tathimini hiyo viongozi na wasimamizi wa miradi hiyo
wametakiwa kutimiza ahadi zao kwa kukamilisha miradi hiyo kwa wakati.
No comments:
Post a Comment