Timu ya Simba SC imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya JKT Tanzania leo.
Simba SC imepata ushindi huo mnamo dakika ya 90 zikiwa zimeongezwa 7 kupitia kwa Hassan Dilunga aliyeingia kipindi cha kwanza akichukua nafasi ya John Bocco.
Ushindi huo unaifanya Simba kufikisha pointi 72 wakibaki nafasi ya pili huku Yanga akiwa bado kileleni na pointi zake 77.
No comments:
Post a Comment