A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Tuesday, April 23, 2019

Rais Magufuli aiongezea muda Bodi ya Utalii Tanzania (TTB)

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ameongeza muda wa miaka 3 kwa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) iliyokuwa imalize muda wake leo tarehe 23 Aprili, 2019.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa Mwenyekiti na Wajumbe wote wa bodi hiyo  wameongezewa muda hadi tarehe 23 Aprili, 2022.

Bodi hiyo inaongozwa na Mwenyekiti, Jaji Mstaafu Thomas Mihayo na wajumbe 6 kama ifuatavyo;

Bw. Augustine Kungu Olal.
Bi. Zabein Muhaji Mhita.
Bw. Richard Rugimbana.
Bw. Mark Leveri.
Bw. Ally Hussein Laay.
Bw. Ibrahim Mussa.


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages