Kundi la itikadi kali linalojiita "Dola la kiislam" IS, limedai kuhusika na mashambulio ya kujitoa mhanga maisha yaliyotokea makanisani na katika hoteli za kifahari na kuangamiza maisha ya zaidi ya watu 320 mnamo Jumapili ya Pasaka nchini Sri Lanka.
Kupitia shirika lake la kueneza propaganda, Amaq, kundi hilo limesema mashambulizi hayo yaliwalenga raia wa zile nchi zinazounda muungano dhidi ya IS pamoja na wakristo wa Sri Lanka.
Watu walioyatoa mhanga maisha yao walijiripua katika hoteli tatu za kifahari na makanisa matatu, wakati wa misa mjini Colombo na katika miji mengine ya Sri Lanka.
Waziri Mkuu wa Sri Lanka Ranil Wickremesinghe amesema mashambulizi hayo yana uhusiano na IS. Viongozi wa serikali wamewatwika jukumu la umwagaji damu huo, wanamgambo wa itikadi kali wa Thauheed Jamaath ambao mpaka sasa bado hawajatamka kama walikuwa nyuma ya mashambulio hayo au la.
Post Top Ad
Your Ad Spot
Tuesday, April 23, 2019
IS yadai kuhusika na mashambilizi ya Sri Lanka
Tags
KIMATAIFA#
Share This
About kilole mzee
KIMATAIFA
Labels:
KIMATAIFA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Your Ad Spot
No comments:
Post a Comment