A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Sunday, January 20, 2019

Tshisekedi atangazwa mshindi wa uchaguzi wa rais na Mahakama DRC

Mahakama ya kikatiba ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Jumapili imemtangaza Felix Tshisekedi kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais na kutupilia mbali madai ya Fayulu kwamba uchaguzi huo ulikuwa na udanganyifu.

Uamuzi huo wa kuthibitisha kuwa Tshisekedi ndiye aliibuka mshindi wa kinyang'anyiro hicho cha urais unakuja baada ya mahakama kupinga kesi iliyowasilishwa na kiongozi wa muungano wa upinzani wa LAMUKA Martin Fayulu, licha ya kuwa na mashaka makubwa ya kuwepo udanganyifu wa kura.

Fayulu anadai kwamba Tshisekedi na Rais Joseph Kabila walifanya mpango wa kisiri siri baada ya matokeo ya awali kuonesha kwamba mgombea ambaye alikuwa akiungwa mkono na Kabila, Emmanuel Ramazani Shadary, ameshika nafasi ya tatu katika uchaguzi huo.

Uamuzi huo wa mahakama unamaanisha kuwa sasa Tshisekedi anaweza kuapishwa kuwa rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ifikapo Jumanne wiki ijayo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages