A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Saturday, August 18, 2018

Makonda awaahidi makubwa wasanii


Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda leo ameungana na maelfu ya wakazi wa jiji hilo kwenye Tamasha kubwa la Burudani Komaa Concert 2018 lililoandaliwa na kituo cha utangazaji cha E FM/TV E ambapo amesema serikali ya mkoa huo itaendelea kutoa ushirikiano kwa wasanii kwakuwa sanaa ni Ajira rasmi inayowasaidia vijana wengi.

Akizungumza na maelfu ya wananchi hao Makonda amewaomba waendelee kumpa ushirikiano wa kutosha Rais Dkt. John Magufuli huku akipongeza maendeleo makubwa yaliyopatikana tangu Serikali ya awamu ya tano ilipoingia madarakani.

Aidha Makonda amewapongeza E FM kwa kuandaa tamasha hilo lililotoa fursa kwa wananchi wanyonge kupata burudani huku akiwakumbusha wananchi kuhakikisha wanafanya Usafi wa mazingira wanayoishi.

Pamoja na yote Makonda amewahimiza wananchi kuhakikisha wanalinda Amani, usalama na kuwakumbuka kwenye Maombi viongozi wote wa Taifa.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages