Mvua kali zilizonyesha mjini Abidjan zimesabisha vifo vya watu wawili nchini Ivory Coast.
Mvua kali zimenyesha mjini Abidjan kuanzia Alkhamis hadi Ijumaa na kusababisha maafa na uharibifu wa mali. Taarifa kuhusu mvua hizo mjini Abidjan imetolewa na serikali Jumamosi.
Wizara ya mambo ya ndani na wizara ya ulinzi zimefahamisha kuwa zoezi la kuwaokoa raia ambao wameathiriwa na mvua hizo zinaendelea kote mjini Abidjan.
Waathirika wa mvua hizo ni raia wenye maisha duni wanaoishi katika maeneo ambayo miundombinu haina vigezo vya kumudu mvua.
No comments:
Post a Comment