Wakati Dunia nzima ikisubiri kwa hamu kujua sehemu watakayofanyia
Fungate (Honey Moon) wanandoa wa familia ya kifalme, Prince Harry na
mkewe Meghan Markle hatimaye kitendawili hicho kimeteguliwa.
Kwa mujibu wa watu wa karibu wa familia hiyo ya Kifalme waliohojiwa na
mtandao wa TMZ wameeleza kuwa wawili hao wataenda nchini Canada kwa
ajili ya fungate.
Taarifa hizo zinakuja baada ya mvutano wa muda mrefu kuwa ni wapi wawili
hao wataenda kupumzika baada ya kufunga ndoa huku mitandao mingi
ikizitaja nchi za Afrika.
Mtandao wa TMZ pia umeeleza kuwa tayari wawili hao watafikia katika
Hoteli ya kifahari ya Alberta’s Fairmont Jasper Park Lodge, ambapo bei
ya Chumba (Outlook Cabin) ni Dola za $6,000/= sawa na tsh Milioni 12
kwa usiku Mmoja.
Hii sio mara ya kwanza kwa familia hiyo ya Kifalme kufikia kwenye hoteli
hiyo ya Kifahari kwani mwaka 2005 Malkia Elizabeth II na Prince Philip
walifanyia Honey Moon kwenye Hoteli hiyo.
Post Top Ad
Your Ad Spot
Tuesday, May 29, 2018
Home
KIMATAIFA
Hii ndio nchi ambayo Prince Harry na mkewe Meghan watapumzika kwaajili ya ‘Honey Moon’
Hii ndio nchi ambayo Prince Harry na mkewe Meghan watapumzika kwaajili ya ‘Honey Moon’
Tags
KIMATAIFA#
Share This
About kilole mzee
KIMATAIFA
Labels:
KIMATAIFA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Your Ad Spot
No comments:
Post a Comment