A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Thursday, May 10, 2018

CHADEMA TAIFA BARA NA VISIWANI WAFANYA ZIARA UKONGA

Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Mwita waitara (kushoto) akivuka kivuko cha muda mfupi cha mto Mzinga jijini Dar es Salaam jana pamoja na Viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Taifa katika ziara ya uzindua rasmi wa operesheni ya kusajili wanachama wapya na Ukaguzi wa Miundo mbinu iliyoharibika pamoja na kuangalia maendeleo ya ujenzi wa Daraja la Mto Mzinga lililopo Kivule.Wapili kushoto ni  Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe.
Diwani wa kata ya Kivule,Wilson Molel (kushoto) akiwaeleza jambo viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Taifa maafa ya mvua za hivi kati zilivyoathiri miundo mbinu ya kata ya Kivule.
Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Mwita Waitara (kulia) akiwaeleza jambo viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Taifa jijini Dar es Salaam jana baada ya kuwasili katika jimbo la Ukonga hilo kata ya Kivule kwa ajili ya Ukaguzi wa miundo mbinu iliyoharibika, kutoa pole kwa wahanga wa maafa ya mvua na kuangalia maendeleo ya ujenzi wa Daraja la Mto Mzinga lililopo Kivule. Uongozi wa Chadema Taifa ulizindua rasmi operesheni ya kusajili wanachama wapya katika Jimbo la Ukonga na baadae mikoa mingine nchi nzima bara na visiwani.Katikati ni Katibu Mkuu Chadema,Vincent Mashinji na  Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),  Freeman Mbowe (kushoto) akizungumza na wakazi wa kata Kivule jijini Dar es Salaam jana baada ya Kuwasili katika kata hiyo na Viongozi wa Chadema Taifa kwa ajili ya Uzinduzi rasmi wa Operesheni ya Kusajili wanachama wapya wa jimbo la Ukonga na baadae mikoa mingine nchi nzima bara na visiwani. Vilevile uongozi wa Chadema Taifa umefanya Ukaguzi wa miundo mbinu iliyoharibika,kutoa pole kwa wahanga wa maafa ya mvua na kuangalia maendeleo ya ujenzi wa Daraja la Mto Mzinga lililopo Kivule.Katikati  ni Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Mwita Waitara.
Viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Taifa wakishuka katika mtumbwi uliotengenezwa kienyeji unaofanya kazi ya kuvusha wakazi wa Kivule katika Mto Mzinga.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),  Freeman Mbowe (kushoto), Makamu Mwenyekiti wa Chadema Tanzania Bara, Professa Abdallah Safari,Makamu Mwenyekiti Zanzibar, Saidi Issa Mohamed pamoja na Viongozi wengine wa Chama wakiongoza baada ya kumaliza ziara.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages