Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda anawatangazia
wananchi wote waliowasilisha Malalamiko yao kwenye Ofisi yake dhidi ya Taasisi
za Kifedha na Bank kufika Ofisini kwake siku ya kesho March 02 kuanzia Saa
mbili asubuhi kwaajili ya kuchukuwa Majibu yao.
Walengwa ni wale waliosikilizwa na jopo la wataalamu na wanasheria
wakati wa Wiki ya RC Makonda kutoa Masaada wa kisheria kwa wanyonge iliyofanyika
January 29 hadi February 03.
Zoezi la kutoa majibu linaendelea ambapo leo ilikuwa ni zamu ya
wananchi wenye malalamiko dhidi ya Kazi na Ajira pamoja na Mirathi.
No comments:
Post a Comment