Timu ya Simba imewakalisha wapinzani wao wa jadi Yanga kwa mapato jumla
ya fedha walizoweza kuingiza katika mechi zao za kimataifa zilizochezwa
katika siku mbili tofauti ndani ya dimba la Taifa Jijini Dar es Salaam.
Hayo yamebainishwa na taarifa zilizotolewa na uongozi wa Shirikisho la
Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na kusema mechi ya Simba dhidi ya Al Masry
ya Misri uliochezwa Jumatano Machi 7,2018 umeweza kuingiza takribani
milioni 85 katika fedha zote huku mashabiki elfu kumi na nne mia saba
tisini na nane (14,798) wakiwa wamehudhuria kuangalia mtanange huo
uwanja wa Taifa.
Kwa upande wa mchezo wa Yanga umeweza kuingiza mashabiki elfu tisa mia
tisa sitini na moja(9,961) na kufanikiwa kukusanya zaidi ya fedha
milioni 56 za kitanzania katika mchezo wake dhidi ya Township Rollers ya
Botswana uliochezwa Jumanne Machi 6,2018.
Kwa upande mwingine, TFF imesema baada ya kumalizika kufanyika kwa
mgawanyo wa pesa hizo zote kwa kila mechi timu ya Simba ikapata
takribani milioni 43 za kitanzania huku Yanga wakiramba takribani
milioni 28 za pesa zote zilizoweza kukusanywa
Post Top Ad
Your Ad Spot
Friday, March 9, 2018
Simba SC Yaingiza Mkwanja Mrefu Zaidi Ya Yanga
Tags
MICHEZO#
Share This
About kilole mzee
MICHEZO
Labels:
MICHEZO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Your Ad Spot
No comments:
Post a Comment