Tazama matukio katika picha maadhimisho ya siku ya Usonji (AUTISM) yaliyofanyika katika Shule ya Almuntazir Islamic leo jijini Dar es Salaam, na kuhudhuriwa na Naibu spika wa Bunge Mhe. Tulia Akson, Na Naibu waziri wa Afya Maendeleo Jinsia wazee na Watoto Dr. Faustin Ndungulile pamoja na wabunge mbalimbali wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
Naibu Spika wa Bunge Tulia Akson akikata utepe kufungua matembezi ya siku ya usonji yaliyofanyika leo ambapo yameanza barabara ya Obama katika Shule ya Wavulana Almutazir hadi katika Shule ya wasichana iliyopo bahari beach Jijini Dar es Salaam.
Makumu MKuu wa Shule ya wasichana Almuntazir Mrs. Joan akitoa utaratibu wa shughuli mbalimbali katika
Naibu spika wa Bunge la jamuhuri ya Tanzania Tulia Akson,akipokea Zawadi iliyoandaliwa Na Almuntazir School ambapo itakuwa ni ukumbusho wa kukumbuka siku hii muhimu ya watu wenye uhitaji maalumu (AUTISM).
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Maendeleo na Watoto Dr. Faustin Ndungulile Akipokea Zawadi kutoka SHule ya Almuntazir.
Watoto wenye uhitaji maalum, wakiimba nyimbo katika maadhimisho ya siku ya Usonji Duniani ambapo yamefanyika katika Shule ya Almuntazir Islamic school, leo jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment