A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Wednesday, March 7, 2018

Shamsa Ford afunguka ishu ya kutojichanganya na wenzake

KUMEKUWA na matukio mbalimbali yanayowakusanya wasanii, lakini tofauti na zamani, Shamsa Ford kwa sasa amekuwa haonekani akijichanganya na wenzake, jambo ambalo limezua minong’ono na kusababisha mwenyewe kuibuka na kudai kuwa jambo hilo lilisababisha mimba yake changa ikachoropoka.

Shamsa aliiambia Za Motomoto News kuwa, awali alikuwa akijichanganya mno kwenye ishu tofauti, lakini kwa sasa anashindwa kutokana na kupigwa marufuku na mumewe, Chid Mapenzi, baada ya kuwa na ujauzito mchanga ambao ulichoropoka kwa sababu ya kuzurura.

“Nilipigwa marufuku kutokatoka licha ya kwamba mwanzoni nilikuwa ninatoka kibishibishi tu, lakini kwa sasa imenibidi nimsikilize mume wangu zaidi maana mimba changa ilitoka kwa sababu ya kutokatoka hovyo kwenda kwenye shughuli,” alisema Shamsa.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages