A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Thursday, February 1, 2018

Binti Filam Fondation imetoa msaada wa milioni 30 hospital ya mwananyamala

Uongozi wa Taasisi ya Binti filamu Fondation umetoa Msaada wa Vifaa tiba vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 30 katika hospitali ya Mwananyamala Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es salaam.

Meya  wa Kinondoni akizungumza na wadau na kutoka Taasisi ya Binti Filamu Fondution.

Akizungumza Jijini Dar es salaam leo Mstahiki Meya Manispaa hiyo Benjamin Sitta amesema,ameushukuru uongozi huo,kwa kutoa msaada huo katika hospitali hiyo na kusema kuwa kitendo hicho kimeonyesha ukomavu katika sekta ya filam kwa kutumika ipasavyo katika jamii na kuleta matokeo mazuri.


Amesema  wasanii wanauwezo mkubwa wa ushawishi katika makundi tofauti katika jamii na kusema kuwa kama watatumika vizuri wataleta maendeleo makubwa .

"Upo uwezekano kwa wasanii wa filamu nchini na wasanii wa aina zote wakatumika positively (vizuri) kwenye jamii na wakaleta impact (matokeo)kubwa" amesema Sitta

Aidha Sitta amesema tukio hilo liwe chachu kwa wasanii wa aina nyingine ili wajue kuwa nguvu yao katika jamii ni kubwa na sio kufanya matukio kwenye mitandao ya kijamii.

"matukio wanayo yafanya yanaleta athari kubwa kwa hawa vijana wadogo ambao tunawahangaikia wapate elimu bure, wasome  wanaendelea kukosa mwelekeo kwasababu wanaona Role Models wao mafanikio yao wanayapeleka kwenye mambo ya ajabu ajabu na kibaya zaidi sikuhizi kitu kidogo kwenye mitandao kinaenea kwa haraka zaidi  "Amesema Sitta

Hata hivyo Siitta amewaahidi kuwapa ushirikiano katika nyanja tofauti kwa kuwakutanisha na wadau watakao watakaowahitaji hivyo amewataka kuleta mawazo yao yatakayofaa kwa manufaa ya jamii nzima.

Kwa upande wake Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo Dr. ISDORY KIWALE  ametoa shukrani zake za dhati  kwa uongozi wa Tasisi hiyo kwa msaada huo na kusema kuwa sio mara yao ya kwanza kufika hospitalini hapo na kutoa msaada hivyo wamekuwa na mchango mkubwa katika Hospitali hiyo.

"Mwaka jana tulikuwa na shida ya Damu hivyo Wasanii hao walijitokeza na kuchangia Damu lakini na leo wamefika hapa na kutupatia vifaa tiba vyenye thamani ya zaidi ya shilingi Milioni 30 na sisi tunawaahidi vifaa hivi vitatumika kwa uangalifu mkubwa sana"Amesema Dr ISDORY

Amesema pamoja na jitihada kubwa zinazofanywa na serikali bado wanahitaji watu ili wawasaidie katika nyanja tofauti za kuwapatia  vifaa tiba.

Mlezi wa Taasisi hiyo Mama Asha Baraka akizungumza katika hafla hiyo

Kwa upande wake Mlezi wa Taasisi hiyo Mama Asha Baraka amesema  kuwa lengo lao kubwa ni kuisaidia jamii ,hasa akina mama na watoto ambapo pia ni harakati za kumuunga Mkono  Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli kwa  kuwapa vipaumbele wazee na akina mama wasio na uwezo.


MATUKIO KATIKA PICHA











No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages