Meneja Mawasiliano wa Tigo, Woinde Shisael (kulia), akikabidhi
fungua ya Pikipiki aina ya Hero kwa Pius Kavike, mmoja kati ya washindi nane (8)
waliojishindia pikipiki nne pamoja na
televisheni nne za LED flati skrini kwenye promosheni ya Nunua Simu ya Tecno R6,S1
na Ushinde, Makabidhiano hayo yamefanyika Makao Makuu ya Tigo jijini Dar es
Salaam leo.
Meneja Mawasiliano wa Tigo, Woinde Shisael, akiongea na
waandishi wa habari wakati akikabidhi zawadi kwa washindi waliojishindia
pikipiki nne pamoja na televisheni nne za LED flati skrini kwenye Promosheni ya Nunua Simu ya Tecno
R6,S1 na Ushinde, Makabidhiano hayo yamefanyika Makao Makuu ya Tigo jijini Dar
es Salaam leo
.
Meneja Mawasiliano wa Tigo, Woinde Shisael (kulia),
akikabidhi fungua ya Pikipiki aina ya Hero kwa Tumaini Massra, mmoja kati ya washindi nane
(8) waliojishindia pikipiki nne pamoja
na televisheni nne za LED flati
skrini kwenye promosheni ya Nunua Simu
ya Tecno R6,S1 na Ushinde, Makabidhiano hayo yamefanyika Makao Makuu ya Tigo
jijini Dar es Salaam leo.
Tigo Yatoa Zawadi kwa Washindi wa Promosheni ya ‘Nunua Simu na Ushinde.”
Wateja wajinyakulia pikipiki 4 na televisheni 4 za LED katika droo ya wiki hii.
Dar es Salaam, Septemba15, 2017- Kampuni inayoongoza kwa
mageuzi ya kidigitali nchini, Tigo Tanzania, leo imetoa pikipiki nne (4) na
televisheni nne (4) za LED flatscrini kwa washindi wa promosheni yake
inayoendelea nchini nzima ya ‘Nunua Simu na Ushinde’.
Akizungumza
katika hafla ya kukabidhi zawadi kwa washindi iliyofanyika katika ofisi za
Tigo, jijini Dar es Salaam leo, Meneja Mawasiliano wa Tigo, Woinde Shisael
aliwatangaza washindi wa pikipiki kuwa ni Tumaini Massra (kinyozi) na Pius
Kivike (fundi) wa Dar es Salaam, Restituta Gervas wa Mwanza na Moses William wa
Sumbawanga. Washindi wa wiki hii wa luninga za LED flatscrini ni Bahati
Sambayuka wa Dar es Salaam, Venanty Ndunguru wa Mtwara, Jackson Mwenga wa Mbeya
na Amuri Kalinga wa Iringa.
Akiwapongeza washindi,
Woinde alisema kuwa Tigo inaongoza katika mageuzi ya kidigitali nchini na ndio
maana inawapa wateja wake fursa ya kumiliki simu bora za kisasa kwa bei nafuu,
pamoja na kuwapa nafasi ya kushinda zawadi zitakazoboresha maisha yao.
‘Huu ni muendelezo wa
juhudi za Tigo kukuza mabadiliko ya digitali nchini. Kwa manunuzi ya simu aina
ya Tecno S1 na Tecno R6 kutoka maduka yote ya Tigo nchini, wateja wanaingizwa
kwenye droo inayowapa nafasi ya kushinda mojawapo ya pikipiki 14 na televisheni
14 za kisasa ambazo bado zinazoshindaniwa kwenye promosheni hii,’ aliongeza.
Promosheni hii ya Tecno S1 na Tecno R6 inahusu tu wale
wateja watakaonunua simu za aina hii kutoka kwa maduka ya Tigo nchini kote.
Simu ya Tecno S1 ni ya mfumo wa 3G na inapatikana kwa bei ya shilingi 99,000/-
tu. Simu ya Tecno R ni ya mfumo wa 4G na inapatikana kwa bei ya shilingi
195,000/- tu.
‘Simu zote mbili ni za kisasa na zina uwezo wa kutumia
mfumo wa data, kwa hiyo wateja wataweza kutumia huduma bora za data za 3G na 4G
kutoka Tigo, hii ikiwa inalingana na aina ya simu watakayonunua’ Woinde alifafanua.
...........................................................................................................................
Kuhusu
Tigo:
Tigo
Tanzania ni kampuni ya simu inayotoa huduma bora za maisha ya kidigitali nchini
Tanzania. Tigo ilianza kuendesha shughuli zake nchini Tanzania mwaka 1994.
Kupitia
huduma zake za kipekee za sauti, ujumbe mfupi, intaneti yenye kasi na huduma za
kifedha kupitia simu za mikononi, Tigo inaongoza kwa ubunifu wa kidigitali kwa
kuwa kampuni ya kwanza Tanzania kuzindua facebook na smartphone zenye lugha ya
Kiswahili, huduma ya TigoPesa, pamoja na huduma ya kwanza inayowezesha wateja
kufanya miamala ya fedha kupitia simu za mkononi kwenda nje ya nchi yenye uwezo
wa kubadili thamani ya fedha kwa sarafu ya nchi husika Afrika Mashariki.
Tigo
ni kampuni ya pili kwa ukuwa nchini na imekuwa kampuni ya simu inayokuwa kwa
kasi zaidi nchini kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo. Kupitia mkakati
mkubwa wa kupanua na kuboresha huduma zake, kati ya mwaka 2015 hadi 2016, Tigo ilizindua mtandao wa 4G LTE jijini Dar es
Salaam na katika miji mingine 22 nchini.
Tigo
inajivunia jumla ya watumiaji milioni 10 wa simu waliosajiliwa, na imetoa
nafasi za ajira za moja kwa moja na zile zisizokuwa na moja kwa moja kwa
Watanzania wapatao 300,000; hii ikiwa ni pamoja na wawakilishi wa huduma kwa
wateja, wafanyabiashara wakubwa wa fedha kupitia simu za mikononi, mawakala wa
mauzo na wasambazaji.
Tigo
ni nembo ya kibiashara ya Millicom, kampuni ya kimataifa inayoongoza mageuzi ya
maisha ya kidigitali katika nchi 13 duniani. Ikiwa inaendesha shughuli zake za
kibiashara katika bara la Afrika na Amerika ya Kusini, Ofisi kuu za Millicom
zipo Ulaya na Marekani.
………………………………………………………………………………………………………
Kwa
taarifa zaidi tembelea: www.tigo.co.tz au wasiliana na:
Woinde
Shisael – Meneja Mawasiliano
Simu:
+255 713 123431 Barua pepe:
Woinde.shisael@tigo.co.tz
No comments:
Post a Comment