Mkuu wa Mkoa
wa Dar es Salaam, Paul Makonda, wa tatu (kushoto) akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa
ujenzi wa ofisi 402 za walimu katika Mkoa
wake, uzinduzi huo umefanyika katika viwanja vya Gereza la Ukonga jijini hapa
leo, wapili (kushoto) ni Mwenyekiti wa kamati ya ujenzi wa ofisi hizo Kanali
Charles Mbuge, na wengine ni baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo.
Mkuu wa Mkoa
wa Dar es Salaam, Paul Makonda, akizungumza na waandishi wa habari wakati wa
uzinduzi rasmi wa ujenzi wa ofisi 402 za walimu katika Mkoa wake, uzinduzi huo umefanyika katika
viwanja vya Gereza la Ukonga jijini hapa leo, wapili (kushoto) ni Mwenyekiti wa
kamati ya ujenzi wa ofisi hizo Kanali Charles Mbuge, na wengine ni baadhi ya
wajumbe wa kamati hiyo.
Mwenyekiti wa
kamati ya ujenzi wa ofisi 402 za walimu Mkoa wa Dar es Salaam, Kanali Charles
Mbuge, akizungumza katika hafla hiyo.
Makonda akisalimiana na wajumbe wa kamati ya ujenzi
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda amezindua rasmi ujenzi wa ofisi za walimu 402 kwa Mkoa huo, huku akiwataka wananchi na wadau wengine kuunga mkono jitihada hizo.
Makonda ameyasema hayo leo alipotembelea katika eneo ambalo limetengwa maalumu kwa shughuli za ufyatuaji wa tofali Ukonga Magereza jijini humo.
Amesema watahakikisha ndani ya wiki hii inapatikana mifuko ya saruji zaidi ya elfu kumi (10000) sambamba na mafuta ya kuweza kusukumia mitambo ya kufyatulia matofali.
Nae Kanali Charles Mbuge ambae ni Mwenyekiti wa kamati ya ujenzi wa ofisi za walimu,ameelezea mafanikio waliyo yapata katika michango ya ujenzi huo ni milioni mia mbili ishirini na saba, laki tatu ,ishirini sita elfu na mia mbili.
Aidha ameelezea changamoto walizonazo ikiwamo ya kutoka katika baraza la mazingira NEMC kuhusu uchimbaji wa mchanga katika mto mpiji, upungufu wa mafuta wa mara kwa mara ,upungufu wa malori unaosababisha kushindwa kufanya kazi nyakati za usiku ambapo kazi hizo hufanywa usiku na mchana ,upungufu wa vibao vya kufyatulia tofali ,ambapo idadi inayohitajika ni vibao elfu kumi, sambamba na ukosefu wa magari ya utawala.
"Mkuu wa Mkoa ametoa wazo la kusimamia maendeleo hayo kwa sababu anawapenda watanzania wote hasa wana Dar es salaam"Alisema Kanali Charles.
Aidha amewasa wadau na wapenda maendeleo kuendelea kusaidia ili kutatua changamoto hizo na kufanikisha mradi huo wenye tija kubwa kwa Taifa.
No comments:
Post a Comment