A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Friday, September 29, 2017

RC: MAKONDA ATILIA MKAZO SWALA LA VIWANDA

Vyama vya ushirika jijini Dar es salaam  vimetakiwa kutumia ushirika huo  kuanzisha viwanda vidogo ili kumuunga mkono Rais wa jamhuri ya muuungano wa Tanzania  mhe. John  Pombe Magufuli katika ujenzi wa Tanzania ya viwanda na  kukuza uchumi wa wananchi na kutengeneza ajira kwa watanzania.
Mkuu wa mkoa wa Dar essalaam mhe. Paul  Makonda akitoa hotuba ya ufunguzi wa mkutano Kauli hiyo imetolewa na  mkuu wa mkoa wa Dar es salaam mhe. Paul Makonda wakati wa ufunguzi wa mkutano wa jukwaa la wana ushirika  mkoa wa Dar es salaam uliofanyika Wilayani  Kigamboni , na kuwasisitiza wana ushirika hao kushiriki katka shughuli za maendeleo ya koa huo ikiwemo kuchagia ujenzi wa ofis za walimu.
Aidha Makonda  amwaetaka wanaushirika hao  kuzingatia sheria, kanuni na tatatibu za kuanzishwa kwake ili kufikia malengo walojiwekea katika vyamahiyo.

Vilevile Miongoni mwa Changamoto zilizotajwa  kurudisha nyuma maendeleo ya  Ushirika ni pamoja na Makato makubwa ya Fedha, Kucheleweshwa kwa Marejesho, Wakopaji kushindwa kulipa madeni na kukimbilia kuweka zuio la kufilisiwa mali Mahakamani na Baadhi ya Waajiri kutowasikisha makato na marejesho ya Wanachama waliokopa.
 Hata hivyo  Kuhusu Changamoto hizo  RC Makonda  amewataka Viongozi kuziandika Changamoto hizo kisha kumpatia ili aziwasilishe kwenye ngazi husika ili ziweze kupatiwa ufumbuzi.

Katika mkutano huo pia wanachama walipata fursa ya kupiga kura na  ku mchagua mwenyekiti ,ambapo  Tumain Wilfred   alichaguliwa na mara baada ya kucha guliwa ameeleza namna atakavyo itumika nafasi huku akiweka wazi mabo yaliyolisababisha vyama vya ushika nchini kurudi nyuma  kuwani udhaifu wa sheria ambapo sas imetungwa sheria kali inayo weza kuwabana viongozi  wabadhirifu wa mali za ushirika .
Pamoja na hayo wana ushirika wa  mkoa huo wameiomba serikali  kupunguza tozo kwa vyama hivyo ambavyo vina mtaji chini ya  milioni 150  ili viweze kupiga hatua kimaendeeleo  ,Mkoa wa Dar es salaam una jumla ya Vyama 763 vyenye wanachama zaidi ya 238,897.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages