Timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu ya wasichana wenye umri wa chini ya
miaka 20 ya Nigeria ‘Falconets’ inatarajiwa kutua nchini usiku wa kumkia
Ijumaa Septemba 29, kuvaana na Tanzanite kwenye mchezo wa marudiano
kuwania kucheza fainali za Kombe la Dunia
Mchezo huo wa marudiano utafanyika Jumapili Oktoba mosi, mwaka huu
kwenye Uwanja wa Azam ulioko Chamazi, Dar es Salaam kuanzia saa 10.00
jioni.
Tanzania ina matumaini ya kufanya vema kwenye mchezo huo wa marudio
licha ya kupoteza kwa mabao 3-0 katika mchezo wa kwanza uliofanyika
Uwanja wa Samwel Oigemudia ulioko Jimbo la Benin, Nigeria.
Timu hiyo ya wasichana yenye wachezaji 18, watatua Dar es Salaam saa
9.40 usiku na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, limewapangia kuishi
katika Hoteli ya Urban Rose iliyoko katikati ya jiji la Dar es Salaam
katika kipindi cha siku tatu watakazokuwa hapa jijini.
Aidha kikosi hicho kutokea Nigeria kinatarajiwa kuwa cha watu 31 huku
miongoni mwake wakiwa wako maofisa 13. Fainali za Kombe la Dunia
zitafanyika Ufaransa hapo mwakani
Post Top Ad
Your Ad Spot
Thursday, September 28, 2017
Nigeria kutua Dar kupambana na Tanzanite
Tags
MICHEZO#
Share This
About kilole mzee
MICHEZO
Labels:
MICHEZO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Your Ad Spot
No comments:
Post a Comment