A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Saturday, September 30, 2017

Kinondoni ya saini mikataba ya sh.bilioni 49


Mkurugenzi wa Halmshauri ya Manispaa ya Kinondoni   Aron Kagurumjuli

HALMASHAURI ya Manispaa ya Kinondoni, jijini  Dar es Salaam,  imetiliana saini mikataba miwili  ya ujenzi wa barabara yenye thamani ya sh. bilioni 49  na kampuni za ukandarasi za  Estim Constructions Company Limited ya hapa nchini na  kampuni ya CCEC ya China.


Mstahiki meya wa  Manispaa ya Kinondoni Mh Benjamin Sitta (kushoto),  akitia saini  Mikataba hiyo.

Akizun gumza wakati wa hafka ya utilianaji saini mikataba hiyo, jana, Mkurugenzi wa Halmshauri ya Manispaa ya Kinondoni   Aron Kagurumjuli,   alisema miradi  itakayotekelezwa kupitia  mikataba hiyo ipo chini ya Mradi wa Kuboresha jiji la Dar es Salaam(DMDP).



Mkurugenzi huyo Amesema, Utekelezaji wa miradi hiyo itakuwa kimafungu ambapo  fungu la kwanza lilianza kutekelezwa Desemba  mwaka jana   huku  baadhi ya barabara zilizohusika ni  Makumbusho, Nzasa  pamoja na Soko la Samaki Msasani .

Amesema MIkataba iliyosainiwa leo  inahusisha fungu la pili na la tatu huku  fungu la pili litatekelezwa na kampuni ya  ukandarasi ya CCEC  ikuhusisha barabara za  Makanya, Tandale, Kilongawima, Simu 2000 na  Tandale Kisiwani.

Aidha amesema Barabara hizo  zina jumla ya urefu wa  kilomita  10 na thamani ya ujenzi wake ni sh. bilioni  28. Fungu la  tatu  litatekelezwa na mkandarasi Estim ambapo barabara zitakazo husika ni  Ubungo External, Kisukuru, , Kilungile na Korogwe zenye  jumla ya urefu wa Kilomita 7.5 ambapo  thamani ya ujenzi wake ni sh.bilioni 21.

Kwa upande wa Meya wa Kinondoni, Benjamin Sitta,  alisema mikataba  iliyosainiwa kupitita DMDP itahusisha pia Halmshauri za Manipaa za Ubungo na Ilala.

Meya Sitta amesema   kuwa kwa sababu hiyo  barabara zinaingiliana katika manispaa hizo,huku akiweka wazi  kuwa barabara zitakazojengwa kupitia miradi hiyo ya DMDP ni za kisasa na viwango vya juu.

Amesema katika fungu la  kwanza la ujenzi  umefikia  asilimisa 80 inatekelezwa na kampuni ya Estimu.

amewataka wakandarasi kumaliza utekelezaji wa miradi hiyo kwa  wakati  kutokana na umuhimu wa barabara hizo katika jamii.

Amesema kusainiwa kwa mikataba hiyo   kunatokana na kasi ya  Rais Dk. John Magufuli  ambaye amekuwa akiharakisha shughuli za maendeleo  na msimamo wake wa kutaka watu wafanya kazi.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages