Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Hashim Mgandilwa amewaongoza wafanyabiashara wa
magari (wamiliki wa yadi) katika zoezi la ukaguzi wa eneo maalum lililotengwa
kwa ajili ya ununuzi na uuzaji wa magari kwa mkoa wa Dar es Salaam.
Akizungumza jijini Dar es Salaam na wafanyabiashara hao Mkuu wa Wilaya ya
Kigamboni Hashim Mgandilwa ameeleza kuwa lengo la kuwapeleka wafanyabiashara
hao katika eneo hilo la Kisarawe II Kigamboni ni kuwaeleza namna
watakavyomilikishwa na serikali ina mpango gani na eneo hilo.
Akieleza jinisi watakavyo wamilikisha wafanyabiashara hao DC Mgandilwa
amesema watawapa maeneo hayo bure kwa muda wa miaka mitatu bila malipo ila
watalazimika kulipa kiasi cha shilingi laki tatu kama dhamana ya kuonesha nia,
kisha baada ya miaka mitatu wataanza kulipa kodi ya nusu dola (1250) kwa mwezi
kila baada ya miezi sita.
DC Mgandilwa ameongeza kuwa wafanyabiashara hao wakitaka kukodi maeneo hayo
watalazimika kulipia kiasi cha shilingi 30000 kwa mita mraba moja ndani ya
miezi mitatu, lakini pia wakitaka kununua kwa mwaka watalazimika kulipa 35000
kwa mita mraba moja ndani ya miaka mitatu.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Property International Limited Halim Zaharani
amesema eneo walilotenga kwa ajili ya shughuli hiyo ya yadi ya kuuzia magari ni
mita za mraba 750,000 na wameweka ziada ya mita mraba zaidi ya 300,000.
Naye mmoja wa wafanyabiashara waliofika eneo hilo Salim
Chicago amepongeza kuanzishwa kwa mpango huo wa yadi ya pamoja ambao
ameeleza kuwa utawarahisishia wateja kuwa sehemu moja ambayo inatambulika na
uwepo wa aina mbalimbali za magari, ambapo amebainisha kuwa mfumo huo wa kuwa
na eneo maalum la uuzaji unatumiwa na nchi nyingi zilizoendelea duniani ikiwemo
Dubai, Japan na Singapore.
Uwepo wa eneo hilo ni ushirikiano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam
Paul Makonda na Kampuni ya Property International LTD, eneo hilo lipo umbali wa
Kilomita 16 kutoka daraja jipya la Mwalimu Nyerere na Kilomita 10 kutoka Kibada
Senta na miundombinu muhimu ya kijamii kama barabara, maji, umeme vipo katika
mkakati wa uendelezaji.
Mmoja yawafanya biashara hiyo kwa muda mrefu akitoa neno la pongezi kumpongeza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda. kwa kutoa maeneo hayo kwa wafanya biashara wa magari.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Kigamboni, Rahel Mugando, wa pili (kushoto), akifafanua jambo kwa baadhi ya wafanya biashara wa magari waliojitokeza katika maeneo hayo.
Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Hashim Mgandilwa (kushoto), akifafanua jambo kwa baadhi ya wafanya biashara wa magari waliojitokeza katika maeneo hayo. kushoto kwa Mkuu wa Wilaya ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Kigamboni, Rahel Mugando,
Mafundi umeme wakiwa katika kujenga miundombinu muhimu katika maeneo yatakayojengwa yadi hizo
No comments:
Post a Comment