Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amewataja watu 13 wenye
mitambo ya kufyatua kazi za wasanii wa nje na ndani ya nchi yetu wakutane kituo cha polisi cha kati wakiwa na
nyaraka halali za kufanyia kazi hiyo.
Akizungumza na wasanii hao
pamoja na wananchi leo katika mkutano wa kupambana na maharamia wa kazi za
wasanii,Makonda alisema kuna baadhi ya watu wanafanya kazi za bla bla kwa kuwanyonya
wasanii.
Amesema kuanzia leo ni mwisho kwa wale wanaouza nyimbo za wasanii
amesema wanaotakiwa kufanya hivyo niwale wenye mikataba halali na wasanii wenye
nyimbo husika.
Makonda amesema kuwa kazi zote za wasanii na zinatakiwa ziwe na stika
za Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) ilinchi iweze kupata mapato na kukuza tasnia
ya sanaa nchini.
Amesema kwa wale wanaouza kazi za wasanii mikononi zinatakiwa kuwa na
stika za TRA Pamoja na kuwa na kibali maalum kutoka bodi ya filamu
Hata hivyo amesema Makonda kunawatu wanafanya kazi za kuwarubuni
wasanii na kufanya maisha yao yawe duni katika hiyo wakati Nigeria inaongoza
kwa kupata pesa nyingi kupitia filamu
Mkuu wa Mkoa wa Dar es
Salaam, Paul Makonda akizungumza na wasanii katika mtaa wa Mafya mara baada ya
kumaliza maandamano ya wasanii kupinga uuzwaji wa filamu za nje ambazo
zinachangia kushuka kwa thamani ya filamu za ndani kutokana na bidhaa hizo
kutolipiwa kodi.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala,
Sophia Mjema akizungumza na Wasanii waliofika Kariakoo mara baada ya maandamano
ya kupinga Biashara ya uuzaji filamu za nje.
Katibu Mtendaji wa
Baraza la Sanaa nchini (BASATA), Godfrey Mwingereza akizungumza na wasanii wa
filamu waliofika katika maandamano hayo yaliyoitimishwa katika mtaa wa Mafia
Kariakoo.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda
akiwa katika maandamano na wasanii wa filamu hapa nchini kupinga uuzwaji wa
filamu za nje nchini ambazo hazilipiwi ushuru
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es
Salaam, Simon Sirro akizungumza na Wasanii hao.
Makamu Mwenyekiti wa Shirikisho la Filamu
nchini, Jimy Mafufu akizungumza kwa niaba ya wasanii katika mkutano huo.
Baadhi ya wasanii walishiriki Maandamano hayo
Kundi la Wasanii wakishangilia jambo kutoka kwa
mkuu wa Dar es Salaam Paul Makonda

No comments:
Post a Comment