A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Saturday, April 22, 2017

DIAMOND PLATNUMZ AZINDUA PAFYUM YAKE AINA YA (CHIBU), YAINGIA RASMI KWENYE SOKO, KUPATIKANA MADUKA YOTE YA GSM




Mwanamuziki mashuhuri nchini Tanzania Diamond Platinumz amepiga hatua nyingine baada ya kujitosa katika biashara ya uuzaji wa manukato.



Manukato ya mwanamuziki huyo yamepewa jina Chibu Perfume, kwa kufuata jina lake ya utani la Chibu Dangote.



Chupa ya manukato hayo inauzwa takriban Sh105,000 za Tanzania.



Diamond anaonekana kuwafuata wasanii wengine mashuhuri duniani ambao wamejiingiza katika biashara ya manukato na hutumia umaarufu wa nembo zao kujipatia mapato zaidi.



Wakati wa uzinduzi huo Diamond alisema kuwa ameamua kuingia kwenye soko la kutengeneza manukato 'Pafyum' yenye nembo yake CHIBU ili kusaidia serikali katika suala zima la kutatua changamoto ya uhaba wa ajira nchini lakini pia kuongeza pato la Taifa kwa kulipa Kodi.



Amesema kuwa kuanza kutengenezwa na kuuzwa kwa pafyum hizo kutaongeza ajira kwa vijana wengi lakini pia kutasaidia kukuza uchumi wa nchi kupitia kodi zitakazotozwa kutokana na bidhaa hiyo ambayo wanaume na wanawake wote wanaweza kuitumia, Pafyum ya CHIBU itapatikana katika maduka yote ya GSM na itauzwa bei ya rejareja kiasi cha shilingi 105.000 kwa moja.



Katika mkakati mwingine wa soko, Meneja wa Msanii huyo Bw. Salaam Mendes amesema wako katika mazungumzo na mashirika kadhaa likiwemo shirika la ndege la Kenya Airways kwa ajili ya kuitangaza bidhaa hiyo na kuifikisha kwenye soko la kimataifa ikiwa ni pamoja na kuuzwa katika maduka makubwa kwenye viwanja vya ndege katika nchi mbalimbali ambako ndege za shirika hilo zinafika

Msanii Diamond akifafanua jambo kwa Wanahabari


Manukato hayo yamepewa jina Chibu Perfume



Msanii Nasseb Abdul a.k.a Diamond Platnumz akimkabidhi chupa ya Pafyum, mteja wake wa kwanza aliyejitambulisha kwa jina la Aisha Azori, wakati wa uzinduzi huo.Mwana mama huyo alionekana kujisikia fahari kununua bidhaa ambayo imetengenezwa na Msanii wa hapa nyumbani,ambae pia anafanya vyema katika kazi zake za Muziki,kushototo ni Mmoja wa mameneja wa Diamond Plutnamz almaarufu kwa jina la Babu Tale. 



Msanii wa muziki wa kizazi kipya, ambaye amekuwa akifanya vyema ndani na nje ya nchi (anga za Kimataifa), Naseeb Abdul a.k.a Diamond Platnumz akizungumza mbele ya Waandishi wa habari pamoja na wadau wengine waliohudhuria hafla fupi iliyohusu uzinduzi wa manukato (Pafyum) yake iliyoitwa CHIBU, mapema leo jijini Dar.



Msanii Diamond akionesha moja ya Pafyum yake mbele ya Wanahabari na wadau mbalimbali waliofika kwenye hafla hiyo fupi iliofanyika jijini Dar Es Salaam mapema leo.



Diamond Platumz akiendelea kuzungumza na Wanahabari pamoja na Wadau wake waliofika kulishuhudia tukio la uzinduzi huo.



Mmoja wa Meneja wa Diamond Platnumz almaarufu kwa jina la Babu Tale akiwakaribisha wana habari na wadau mbalimbali waliofika kushuhudia tukio hilo adhimu la uzinduzi wa Pafyum ya msanii huyo iliyojulikana kwa jina la CHIBU.



Msanii Diamond akionesha moja ya Pafyum yake mbele ya Wanahabari na wadau mbalimbali waliofika kwenye hafla hiyo fupi iliofanyika jijini Dar Es Salaam mapema jana.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages