WANAWAKE
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) washeherekea siku ya wanawake na
watoto wa kituo cha Kulelea watoto cha UMRA kilichopo Magomeni Mikumi
Jijini Dar es Salaam.
Akizungumza
leo Machi 8, 2021 wakati wa kukabidhi msaada wa Vitu mbalimbali katika
kituo hicho, Mwanyekiti wa Kamati ya Wanawake Tanesco Makao Makuu,
Prisca Maziwa amesema kuwa msaada huo ni nguvu za pamoja za Shirika
hilo.
Amesema
ikiwa ni kilele cha siku ya kimataifa ya wanawake wameona kusheherekea
pamoja na watoto wa kituo cha MRA ili watoto hao waonje upendo wa mama
ingawa wao hawana wazazi.
"Sisi
tupo karibu na jamii na leo tumekuja kuwatembelea watoto wetu na
kuwaletea mahitaji yatakayowasaidia katika kwa muda kidogo." Amesema
Prisca.
Hata hivyo amewashukuru wafanyakazi wa Tanesco kwa kufanikisha kupata vitu mbalimbali kwaajili ya watoto yatima.
Prisca
ametoa wito kwa watu binafsi mashirika, taasisi mbalimbali kujitoa
kwaajili ya watoto wenye mahitaji na kutowaachia watu wachache kuwalea
watoto hao.
Wafanyakazi
wa Tanesco wanawake makao makuu wamewawakilisha pia wanawake wa vituo
vya kufua Umeme na kampuni Tanzu za Tanesco, wamewasilisha katika kituo
cha UMRA vitu mbalimbali ikiwemo Mchere, sukari, Mafuta, Maharage,
Chumvi, Sabuni na vitu ambavyo vinatumika kijamii.
"Kadiri
Mungu anavyokujalia toa kwenye kituo hicho au vituo vingine kusaidia
katika mahitaji mhimu ya binadamu na kutoa faraja na Upendo kwa watoto
hawa." Amemalizia Prisca.
Kwa
upande wake Mwasisi wa UMRA Orphanage Centre, Rahma Kishumba
amewashukuru wafanyakazi wa Tanesco kwa kutoa misaada mbalimbali kwa
kuweza kuwasaidia ulezi wa watoto.
"Sinabudi
ya kusema wakinamama wa Tanesco Mungu awajalie na awalipe na kila
rakheri na shukrani kwa Mkurugenzi wa Tanesco." Amesema Bi Rahma.
Kwa
upande wa Mwakilishi wa watoto wanaolelewa katika kituo cha UMRA,
Abrakim Mohamed amewashukuru wafanyakazi wanawake wa Tanasco na
kuwaombea yote mema.
Wafanyakazi wa Shirika la Umeme Tanzania wakiwa na watoto wa Kituo cha kulelea watoto Yaztima kilichopo Magomeni jijini Dar es Salaam le Machi 8, 2022 ikiwa ni kusheherekea siku ya wanawake duniani.
Mwanyekiti wa Kamati ya Wanawake Tanesco Makao Makuu, Prisca Maziwa akimkabidhi mtungi wa Gesi Mwasisi wa UMRA Orphanage Centre, Rahma Kishumba leo Machi 8,2022.
Baadhi ya wafanyakazi wa Tanesco wakitoa vinywaji kwa watoto wa Kituo cha UMRA kilihopo Magomeni jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment