Wakurugenzi wa Halmashauri Nchini
 wametakiwa kutenga fedha zitokonazo na faida ya miradi ya kupanga, 
kupima na kumilikisha ardhi kuboresha ofisi za Maafisa Ardhi pamoja na 
kuwanunulia vifaa vya kisasa vitakavyosaidia kuaharakisha zoezi la 
kupanga, kupima na kumilikisha ardhi kwa ufanisi zaidi tofauti na sasa. 
Naibu
 Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi ametoa agizo hilo kwa 
wakurugenzi hao leo mara baada Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi 
Maliasili na Utalii kupokea taarifa ya miradi ya kupanga, kupima na 
kumilikisha ardhi katika Halmashauri ya mji Bunda. 
Halmashauri 
ya mji wa Bunda inatekeleza mradi huo katika vijiji tisa ambapo 
inakusudia kupima, kupanga na kumilikisha viwanja 7,450 baada ya kupokea
 mkopo wa Shilingi M.400.9 zinazotolewa na serikali kupitia Wizara ya 
Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi. 
Naibu Waziri Kikwete 
aliongeza kuwa baadhi ya Wakurugenzi wa Halmashauri wanawathamini 
Maafisa Ardhi wanapokuwa na fedha za miradi lakini miradi hiyo ikiisha 
wanawaweka kando ndio maana ofisi nyingi za maafisa hao ziko katika hali
 mbaya. 
Naibu Waziri huyo pia aliungwa mkono na Mwenyekiti wa 
Kamati hiyo Bw. Ally Makoa ambaye alimwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri 
ya Bunda Emmanuel Mkongo kuboresha Ofisi ya Maafisa ardhi kwa kutumia 
sehemu ya faida itakayopatikana kwenye mauzo ya viwanja mara baada ya 
kurejesha mkopo kwa Wizara ya Ardhi. 
Ripoti ya mradi wa Kupanga,
 kupima na kumilikisha ardhi iliyotolewa na Mkurugenzi Halmashauri Mji 
Bunda Emmanuel Mkungo inasema bada ya kukamilisha zoezi hili inakusudia 
kukusanya Bil. 1.9 zitakazo tokana na mauzo ya viwanja hivyo. 
Kufuatia
 makadilio hayo Mwenyekiti wa Kamati hiyo Munge Ally Makoa akaishauri 
Halmashauri hiyo na nyingine zenye miradi kama hiyo kutumia sehemu ya 
faida hiyo kununua vitendea kazi vya maafisa ardhi na kuboresha 
miundombinu ya Ofisi zao. 
‘’Haiwezekani kwa wanaokuletea kiasi 
hicho cha fedha kufanya kazi katika mazingira magumu wakati ofisi yako 
inatoa kipaumbele katika maeneo mengine.’’ Alisema Ally Makoa Mwenyekiti
 wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Mali Asili na Utalii. 
Mradi
 wa Kupanga, kupima na kumilikisha ardhi unaotekelezwa na Halmashauri 
Mji Bunda unafanyika katika vijiji tisa vya Mbugani viwanja 650,Shuleni 
viwanja 600,Katoriki viwanja 1,000, Ruselu viwanja 700, Kilimani 800, 
Zanziba 300, Balili 1, 200, Idara ya maji 2000 na Guta viwanja 200. 
Halmashauri ya mji Bunda inatekeleza zoezi la Kupanga, Kupima na 
Kumilikisha ardhi katika vijiji hivyo na tayari imeishatumia takriban M.
 100 kwa zoezi linaloendelea na Serikali kupitia Wizara ya Ardhi Nyumba 
na Maendeleo ya Makazi tayari imeisha toa Sh. Bil.50 kukopesha 
Halmashauri 55 nchini ikiwemo Chuo cha Ardhi Morogoro, Dar es Salaam na 
Tabora.
1. Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Ridhiwani Kikwete akikagua vigingi vinavyotengenezwa na Halmashauri ya mji Bunda vitakavyotumika katika Mradi wa kupanga,kupima na kumilikisha ardhi.
1. Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Ridhiwani Kikwete akitoa zawadi kwa Bi.Joyce Nyangoji baada ya kufuraishwa na namna anavyoweza kupanga vigingi kwa ustadi wakati wa ukaguzi wa zoezi la kujenga vigingi vinavyotengenezwa na Halmashauri ya mji Bunda vitakavyotumika katika Mradi wa kupanga,kupima na kumilikisha ardhi.
No comments:
Post a Comment