Stamico wafunika maadhimisho siku ya mwanamke uwanja wa Uhuru
WAFANYAKAZI Serikali na Taasisi zisizo za kiserikali wanawake katika Mkoa wa Dar es Salaam wameungana katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambayo hufanyika kila mwaka Machi 8 kwa kuwa kauli mbiu ya Kizazi cha Haki na Usawa kwa Maendeleo Endelevu.
Katika Maadhimisho hayo wanawake wamesema kuwa kuadhimisha huko ni kuonyesha safari ya mwanamke na kuangalia mafanikio.
Hata hivyo katika maadhimisho haya wanawake wamejitokeza kwa shamlashamla ambazo zinaonyesha maendeleo endelevu yanaonekana.
Wafanyakazi wa Wanawake Shirika la Taifa la Madini (Stamico) wakiwa katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo hufanyika kila Machi 8 ambapo wanawake hao wameonyesha kujiamini katika kutenda kazi kwa maendeleo ya Taifa kama kauli mbiu ya Siku ya Wanawake Duniani Kizazi cha Haki na Usawa katika Maendeleo Endelevu,wafanyakazi hao walikuwa na shamlashala za za namna yake katika katika viwanja vya uhuru jijini Dar es Salaam.
Mmoja ya wafanyakazi wanawake walipotembelea kiwanda chakutengenezea mkaa wa mawe kilichopo msasani jijini Dar es Salaam Latifa Abdallah akiuliza swali kwa Mhandisi Happy Mbenyange wakati walipotembelea kiwanda hicho wakiadhimisha siku ya wanawake Duniani yaliyohitimishwa leo,
Mhandisi wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Happy Mbenyange (kushoto), akitoa maelekezo kwa baadhi ya wafanyakazi wanawake wa Shirika la hilo walipotembelea kiwanda chakutengenezea mkaa wa mawe rafiki kwa mazingira kilichopo msasani jijini Dar es Salaam wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani yaliyohitimishwa leo duniani kote
Na Stella Kessy
KATIKA
Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Shirika la Madini la Taifa
(STAMICO) limetoa pongezi kwa serikali ya awamu ya Sita kwa jitihada za
kuwawezesha Wanawake katika sekta mbalimbali.
Kauli
hiyo imetolewa leo na Mhandisi wa (STAMICO) Pili Athumani amesema
katika shirika la madini limezingatia hilo kwa kuwapa kipaumbele
mwanawake na kutoa majukumu sawa na wanaume ili kutekeleza kauli mbiu
ya Siku ya wanawake.
"Kampuni
yetu inathamini sana wanawake,kwani kwa kulingana na kauli mbiu ya
mwaka huu ni 'kizazi cha haki na usawa kwa maendeleo endelevu kwa
jamii' katika sekta ya madini suala hili limepewa kipaumbele, kwani
wanawake wamekuwa wanapewa kipaumbele katika kusimamia miradi"Amesema.
Ameongeza
kuwa katika sekta ya madini mwitiko wa wanawake umekuwa mwingi katika
shughuli zote za madini Wanawake wengi wamekuwa wakijitokeza na kujiari
na wanazitumikia fursa kama ifuatavyo.
"katika
shirika letu la madini sisi Kama wanawake waandisi tumekuwa tukipewa
majukumu kama wanaume kwahiyo wanaitekeleza hiyo kauli mbiu ipasavyo
kwani tunaopewa miradi mingi ambayo tunasimami na kutendea haki kadri ya
uwezo wetu na kuifanikisha na kutoa matokeo chanya"
Pia ametoa wito kwa serika endelee kutuamini sisi wanawake kwa kupewa majukumu mbalimbali kwani wanawake tunaweza.
No comments:
Post a Comment