A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Wednesday, March 9, 2022

Mzozo wa Ukraine: Nchi za magharibi zakabiliana na Putin 'msumbufu'.

 


_123522586_putin_976getty

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Marais tofauti Wamarekani wametatizika kumkabili Vladimir Putin lakini kwa vile Brussels na Berlin zimejiunga na pambano hilo, sasa hadithi ni tofauti, anaandika Nick Bryant.

Mara nyingi inajaribu kumtazama Vladimir Putin kama kirusi cha milenia lenye umbo la kibinadamu lakini ni hatari kwa usalama.

Rais wa Urusi aliingia madarakani tarehe 31 Desemba 1999, huku ulimwengu ukiwa matumaini kwamba kompyuta zingeharibika wakati saa ilipogonga usiku wa manane, na kushindwa kushughulikia mabadiliko kutoka 1999 hadi 2000.

Kwa miaka 20 sasa, Putin amekuwa akijaribu kuunda aina tofauti ya utendakazi wa mfumo wa kimataifa, kuvuruga utaratibu huria wa kimataifa. Jasusi huyo hodari wa KGB alitaka kurudisha nyuma majira ya saa: kufufua uwezo wa Urusi na kurejesha nguvu na tishio la Umoja wa Kisovieti kabla ya kuvunjika kwake mwaka 1991.

Mwanaharakati huyu wa Urusi amekuwa kiongozi msumbufu zaidi wa kimataifa wa Karne ya 21, mpangaji mkuu wa masaibu mengi kutoka Chechnya hadi Crimea, kutoka Syria hadi jiji kuu la Salisbury. Amejaribu - kwa mafanikio nyakati fulani - kuchora upya ramani ya Uropa.

Amefanikiwa- mara kadhaa -kuuzuia Umoja wa Mataifa. Amedhamiria - kwa mafanikio wakati fulani - kudhoofisha Marekani, na kuharakisha mgawanyiko wake na kupunguza ushawishi wake.

Putin aliingia madarakani wakati wa hali mbaya ya magharibi. Marekani ilikuwa nchi pekee yenye uwezo mkubwa duniani wakati huo. Tasnifu ya Mwisho wa Historia ya Francis Fukuyama, inayotangaza ushindi wa demokrasia huria, ilikubaliwa na wengi.

Baadhi ya wanauchumi hata walitunga nadharia kwamba hakutakuwa tena na visa vya kushuka kwa uchumi, kwa sababu fulani au kwa maslahi ya uchumi mpya wa kidijitali. Pia ilifikiriwa kwamba utandawazi, na kutegemeana uliofanywa, kungezuia mataifa makubwa kiuchumi kupigana vita. Hali hiyo ilijiambatanisha na mtandao, ambao ulionekana kwa kiasi kikubwa kama nguvu ya manufaa ya kimataifa.

_123522706_af1_976getty

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Maelezo ya picha,

Mlinzi wa heshima akisalimiana na Air Force One kwenye lami ya Moscow mnamo 2002

Katika siku za mwanzo haswa, matumaini yale yale yaliyokosewa na mawazo hasi yalibadilisha mtazamo wa magharibi kumhusu Putin- kiungo ambaye sasa ni dhahiri, alikuwa akijaribu kutumia historia kuvunja demokrasia ijapokuwa mchakato huo ulisababisha maafa makubwa.

Marais kadhaa wa Marekani walijipata wakisakata ngoma yake ya kisiasa. Bill Clinton, ambaye alikuwa mkaji wa White House wakati Putin alipoingia madarakani, aliwasilisha aliwasilisha malalamishi hayo ya utaifa kwa kutaka upanuzi wa Nato hadi katika mipaka ya Urusi.

George W Bush hakumuelewa kabisa mwenzake wa Urusi. "Nilimwangalia mwanahume huyo machoni," Bush alisema katika tamko lake maarufu wakati walipokutana mara ya kwanza huko Slovenia mwaka 2001. "Nilimwona moja kama mtu mwaminifu ... niliweza kupata hisia ya nafsi yake." Bush alifikiri kimakosa kwamba angeweza kuanzisha chuki dhidi ya Putin, na kumshawishi kwa upole kurejea katika njia ya kidemokrasia.

Lakini ijapokuwa Bush alizuru Urusi zaidi ya nchi nyingine yoyote-ikiwa ni pamoja na ziarambili za kibinafsi nchumbani kwa Putin huko, St Petersburg - kiongozi huyo wa Urusi tayari alikuwa akionesha mienendo hatari ya kidhalimu.

2008, mwaka wa mwisho wa utawala wa Rais Bush, Putin alivamia Georgia -katika kile alichokitaja kuwa "oparesheni ya utekelezaji wa amani". Kremlin ilihoji wakati huo - na imeendelea kubishana tangu wakati huo - kwamba ilikuwa ni unafiki kwa Washington kulalamika juu ya ukiukaji huu wa sheria za kimataifa baada ya Bush kuivamia Iraq.

_123522705_bush_976getty

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Maelezo ya picha,

George Bush alipomkaribisha Vladimir Putin katika ranchi yake ya Texas...

_123522703_tshirt_976getty

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Maelezo ya picha,

...katika ziara ambayo ilipokelewa na wenyeji kwa vifije

Barack Obama alijitolea kuimarisha uhusiano kati ya Marekani na Urusi. Waziri wake wa kwanza wa mambo ya nje, Hillary Clinton, hata alimpa mwenzake wa Urusi Sergey Lavrov kitufe cha kuweka upya dhihaka (ambacho kiliandikwa kimakosa na neno la Kirusi la "kuzidiwa"). Lakini Putin alijua kwamba Amerika, baada ya vita vyake vya muda mrefu huko Afghanistan na Iraqi, haikutaka tena kuelekeza ulimwengu.

Mwaka 2013 wakati Obama alipokataa kutekeleza onyo lake dhidi ya Bashar al-Assad baaada ya kiongozi huyo wa Syria kutumia silaha za kemikali dhidi ya watu wake, Putin aliona ishara nzuri. Kwa kumsaidia Assad kutekeleza vita vya mauaji aliimarisha ushawishi wa Moscow Mashariki ya Kati wakati Marekani ilikuwa inataka kujiondoa katika eneo hilo. Mwaka uliofuata alinyakua jimbo la Crimea, na kujikita katika eneo la mashariki mwa Ukraine.

Licha ya kuambiwa na Obama "kujiondoa," Putin hata alitaka kushawishi matokeo ya uchaguzi wa urais wa Marekani 2016 kwa matumaini kwamba Hillary Clinton, adui wa muda mrefu, angeshindwa na kwamba Donald Trump, shabiki wa muda mrefu, kijana mpenda anasa angeshinda

Tajiri huyo wa mali ya New York hakuficha kueleza jinsi anavyomvutia Putin, mbinu ya kujipendekeza ambayo inaonekana kumtia moyo zaidi rais huyo wa Urusi. Moscow ilifurahia sana pale Trump alipoikosoa hadharani Nato, akadhoofisha mfumo wa muungano wa Marekani baada ya vita na akawa mchonganishi kiasi kwamba aliiacha Marekani ikiwa imegawanyika zaidi kisiasa kuliko wakati wowote tangu Vita vya wenyewe kwa wenyewe.

_105914180_line976-nc

Urusi yaishambulia Ukraine:Mengi zaidi

_105914180_line976-nc

Bila shaka, basi, lazima turudi nyuma miaka 30 ili kupata kiongozi wa Marekani ambaye mbinu yake kwa Kremlin imekuwa na tija. baada ya kuanguka kwa ukuta wa Berlin Wall, George Herbert Walker Bush alijiepusha na kishawishi cha kufurahia ushindi wa Vita Baridi vya Marekani - kiasi cha mshangao wa kundi la waandishi wa habari wa Ikulu ya Marekani, alikataa kusafiri hadi Berlin kwa mchujo wa ushindi - akijua kwamba ingewaimarisha watu wenye msimamo mkali katika Politburo na wanajeshi wanaotaka kumwondoa Mikhail Gorbachev.

Ukuu huo wa ushindi ulisaidia lilipokuja suala la kuungana tena kwa Ujerumani, ambayo bila shaka ilikuwa mafanikio makubwa zaidi ya sera ya kigeni ya Bush.

Bila shaka Putin ni adui mkubwa zaidi, mgumu zaidi kushughulika naye kuliko hata Leonid Brezhnev au Nikita Khrushchev, Waziri Mkuu wa Usovieti wakati wa Mgogoro wa Kombora la Cuba. Lakini tangu mwanzo wa karne hakuna rais wa Marekani ambaye amekuwa na kipimo chake.

_123522710_clinton_976getty

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Maelezo ya picha,

Bill Clinton alishinikiza upanuzi wa Nato ambao wengine walisema ni makosa

Joe Biden, kama George Herbert Walker Bush, ni shujaa wa Vita Baridi, ambaye amejitolea urais wake kutetea demokrasia ndani na nje ya nchi. Akitaka kuanzisha tena jukumu la jadi la Marekani baada ya vita kama kiongozi wa ulimwengu huru, amejaribu kuhamasisha jumuiya ya kimataifa, kutoa msaada wa kijeshi kwa Ukraine na kupitisha utawala wa vikwazo vikali zaidi kuwahi kulengwa dhidi ya Putin.

Vikosi vya Urusi vilipojikusanya mpakani, pia alishiriki taarifa za kijasusi za Marekani zikionyesha kuwa Putin ameamua kuvamia, kwa njia ambazo zilitaka kuvuruga kampeni za kawaida za upotoshaji za Kremlin na operesheni za uwongo za bendera.

Hotuba yake ya Muungano ikawa kilio cha hadhara. "Uhuru daima utashinda dhuluma," alisema. Na ingawa Biden haongei kwa uwazi au nguvu ya Kennedy au Reagan, hata hivyo ilikuwa hotuba muhimu.

Kinachoshangaza tangu uvamizi wa Urusi kuanza, hata hivyo, imekuwa madai ya uongozi wa rais kutoka mahali pengine. Volodymyr Zelensky amesifiwa na kusifiwa, huku akiendelea na safari hii ya ajabu ya kibinafsi kutoka kwa mcheshi hadi Churchillian colossus.

Huko Brussels, rais wa Tume ya Ulaya, Ursula von der Leyen, amekuwa na uwepo mkubwa. Mwanasiasa huyu wa zamani wa Ujerumani amekuwa msukumo nyuma ya uamuzi huo, kwa mara ya kwanza katika historia ya Umoja wa Ulaya, wa kufadhili na kununua silaha kwa ajili ya taifa linaloshambuliwa, ahadi ambayo inajumuisha sio tu risasi bali ndege za kivita pia.

_123549801_ursula_getty976

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Maelezo ya picha,

Ursula von der Leyen

Mtani wake, Kansela mpya wa Ujerumani Olaf Scholz, pia ameonyesha azma ya kumkabili Putin kuliko mtangulizi wake Angela Merkel. Kwa mwendo wa kasi, amepindua miongo kadhaa ya sera ya kigeni ya Ujerumani baada ya Vita Baridi, mbinu ambayo mara nyingi huelekezwa kwa tahadhari na woga kwa kiongozi wa Urusi.

Berlin imetuma mifumo ya kupambana na vifaru na ndege nchini Ukraine (kukomesha sera ya kutotuma silaha kwenye maeneo ya vita inayotumika), ilisimamisha mradi wa bomba la gesi la Nord Stream 2 Baltic Sea, na kuondoa upinzani wake wa kuizuia Urusi kutoka kwa mfumo wa malipo wa kimataifa wa SWIFT. , na hata kujitolea kutumia 2% ya Pato la Taifa kwa matumizi ya ulinzi.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages