Na.Khadija Seif, Michuzi TV
ALBUM
fupi ya MSANII wa Bongofleva Nasib Abdul maarufu kama Diamond platinum
iliyobeba takribani Nyimbo 10 yasikilizwa Kwa mara ya kwanza katika
ukumbi wa Terrace slipway jijini Dar es salaam.
Album
hiyo iliyobebwa na jina la "Foa" imepokelewa na kuhudhuriwa na Mastaa
mbalimbali ndani na nje ya nchi akiwema Msanii Shodmajozi kutoka Afrika
kusini.
Katika Nyimbo hizo 10 ameweza kushirikisha wasanii kama Zuchu,Mbosso, shodmajozi na Focalist kutokea nchi Afrika kusini.
Aidha,
vibao vinavopatikana kwenye album fupi hiyo ni
Nawaza,okoa,Wonder,Fresh,Sana,Mtasubiri,Fine, Somebody pamoja na Melody
ambapo Kwa Sasa inapatikana kwenye Mitandao yote ya kupakua Muziki.
Diamond
platinum pamoja na Zuchu wakitumbuiza pamoja baada ya kutambulisha
wimbo "Mtasubiri" walioshirikiana katika Album fupi "FOA" iliyoachiwa
rasmi katika ukumbi wa Terrace slipway jijini Dar es salaam.
No comments:
Post a Comment