A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Wednesday, November 24, 2021

RAIS SAMIA AMELETA NEEMA KWA JAMII

 Na Mwandishi wetu Mihambwe


Miradi ya maendeleo inayoendelea kutekelezwa nchi nzima imeleta neema na unafuu mkubwa kwa jamii.

Hayo yamebainishwa na Afisa Tarafa Mihambwe Emmanuel Shilatu wakati alipofanya ziara ya kawaida ya ukaguzi wa miradi wa maendeleo ya Elimu ya ustawi wa jamii kwa Taifa dhidi ya mapambano ya Uviko 19 ambapo amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuleta neema kubwa kwa Watanzania kupitia miradi hiyo.

"Miradi hii ya Elimu si tu inaenda kupunguza tatizo la uhaba wa vyumba vya madarasa bali pia inawaimarisha Wananchi kiuchumi. Mathalani kuna Mafundi viongozi na Masaidia wamepata kazi za ujenzi,wanaingiza fedha; Kuna Wafanyabiashara, Wasafirishaji, Wauzaji vifaa vya ujenzi madukani, Wauzaji vifaa vya kujengea kama vile mawe, kokoto, mchanga nk hawa wote wamepata neema ama fursa ya kufanya biashara, kujiongezea kipato kupitia utekelezaji ujenzi miradi hii ya Elimu na mengineyo. Hivyo kwa niaba ya Wananchi wa Tarafa ya Mihambwe tunamshukuru sana Rais Samia kwa miradi hii inayoenda kuondoa uhaba wa Madarasa na pia amefanya mzunguko wa fedha uongezeke kwa jamii ambapo miradi hiyo inatekelezwa." Alisema Gavana Shilatu.

Gavana Shilatu pia alitumia ziara hiyo kuwasisitiza Mafundi kuongeza kasi zaidi ya ujenzi, kamati za miradi kuhakikisha wanasimamia ubora wa vifaa na ujenzi ili miradi ikamilike kwa wakati, kwa ubora unaolingana na thamani ya fedha.

Tarafa ya Mihambwe imepata fedha toka Serikali kuu Tsh. Milioni 420 kujenga vyumba vya Madarasa 19 kwa shule za Sekondari 5 na vyumba Madarasa 2 kwa shule Shikizi moja. Katika fedha hizo hizo pia wanajenga ofisi 9 za Waalimu na kuweka viti na meza kwenye Madarasa hayo yote 21.



No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages