Charles James, Michuzi TV
ANATOSHA! Ndiyo kauli ambayo
ameitoa Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Shinyanga, Santiel Kirumba
alipokua akimuombea kura Mgombea Ubunge wa Jimbo la Buhigwe, Kavejuru
Felix katika mkutano na wananchi wa kata ya Mahinda.
Akizungumza
katika mkutano huo Mbunge Santiel Kirumba amewataka wananchi wa Buhigwe
kutowachagua wapinzani kwani ni kama watoto wa kambo ambao wamekua
hawaridhiki na jambo lolote linalofanywa na badala yake wamekua watu wa
kulalamika na kupinga maendeleo.
Amesema wakimchagua Kavejuru
wanakua na uhakika wa miradi yao ambayo imeelekezwa kutekelezwa na Ilani
ya Chama cha Mapinduzi kwani anakua na uwezo pia wa kumfikia Rais Samia
na hata Makamu wa Rais Dk Mpango ambaye anatokea jimbo hilo.
“
Msiwape kura wapinzani wao kila siku ni watu wa kulalamika, ni kama
watoto wa kambo ambao wao kila zuri linalofanywa wanasema ni baya,
msimpe kura mpinzani kwani hata hajui namna ya kuonana na Rais wala
viongozi wengine, huyu Kavejuru yeye akiwa anaomba mjengewe barabara
anapiga simu moja kwa moja na inapokelewa.
Naamini Kavejuru
anatosha kuwa mwakilishi wenu bungeni wa kuihimiza serikali ijenge
barabara hapa, iwaletee vituo vya afya lakini pia ni kiungo baina yenu
na serikali katika kuwasemea kwenye miradi ya maji na elimu.
Yaani
nyie watu wa Kigoma ni kama mtoto Mziwanda mna bahati Makamu wa Rais
anatoka kwenu, mna Waziri wa Elimu, Prof Ndalichako hadi Katibu Mkuu
Kiongozi, Balozi Katanga anatoka humu mnataka nini tena watu wa Buhigwe?
tuleteeni Kavejuru aungane na hao wengine kusukuma maendeleo kwa wana
Kigoma,” Amesema Mbunge Kirumba.
Amewataka wa kina Mama
kuwahamasisha wanaume na vijana kuamka alfajiri na mapema kuwahi kwenye
vituo vya kupigia kura siku ya Jumapili Mei 16 na kwenda kuichagua CCM
ishinde kwa kishindo.
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Shinyanga, Santiel Kirumba akipiga magoti kumuombea kura mgombea Ubunge wa CCM Jimbo la Buhigwe, Kavejuru Felix kwenye mkutano na wananchi wa jimbo hilo.
Wananchi mbalimbali waliojitokeza kwenye mkutano wa kampeni za kumnadi mgombea Ubunge wa CCM Jimbo la Buhigwe mkoani Kigoma wakisikiliza Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Shinyanga, Santiel Kirumba akimuombea
No comments:
Post a Comment