A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Thursday, August 20, 2020

KAMPUNI YA UAP INSURANCE TANZANIA YACHANGIA MATANKI KWAAJILI YA SHULE ZA UMMA MKOA WA DAR ES SALAAM

 

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya bima ya UAP, Stephen Lokonyo akionyesha mfano jinsi ya kuosha mikono kwa maji na sabuni kutumia matanki maalumu ya kuoshea mikono yaliyotolewa na kampuni hiyo kwaajili ya Shule za Sekondari na Msingi za Mkoa wa Dar es Salaam katika hafla iliyofanyika jana katika Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa. Kulia ni Afisa Elimu Taaluma Mkoa, Boniphace Wilson na Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari Benjamini Mkapa, Eunice Mganga.
Mkurugenzi Mtendaji wa UAP, Stephen Lokonyo akikabidhi matenki maalumu kwaajili ya kuoshea mikono kwa Afisa elimu taaluma Mkoa wa Dar es Salaam, Boniphace Wilson katika hafla iliyofanyika jana katika Shule ya Sekondari Benjamini Mkapa Dar es Salaam. Kulia ni Mkuu wa Shule ya Minazi Mirefu, Aveline Chugulu. Msaada huo ni sehemu ya kuadhimisha miaka 100 ya utoaji wa huduma za bima Afrika Mashariki.
Mkurugenzi Mtendaji wa UAP, Stephen Lokonyo akipeana mkono na Mwanafunzi wa Kidato cha Kwanza katika Shule ya Benjamini Mkapa, Maliki Salum wakati Kampuni hiyo ilipokabidhi matanki 40 ya kuoshea mikono kwaajili ya shule za Mkoa wa Dar es Salaam. Kulia (mwenye miwani) ni Mkuu wa Shule ya Minazi Mirefu, Aveline Chugulu.
  • Hatua hiyo imelenga kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa wanafunzi na kupunguza hatari ya kusambaa kwa magonjwa.
Dar es Salaam - Katika kuadhimisha miaka 100 ya utoaji huduma kwenye soko la bima, Kampuni ya UAP Insurance Tanzania imetoa msaada wa matanki 40 ya kuoshea mikono kwaajili ya wanafunzi wa shule za msingi na sekondari mkoa wa Dar es Salaam. Hatua hiyo itasaidia kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa wanafunzi.

Matenki hayo yatasiaida kuhakikisha wanfunzi wanapata nafasi ya kunawa mikono yao kwa maji safi na sabuni hivyo kuhakikisha mazingira salama kwa Watoto shuleni. Kampuni hiyo ni kampuni tanzu ya kampuni ya UAP Holdings Plc inayotimiza miaka 100 tangu kuanzishwa kwake mnamo mwaka 1920.

Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi msaada huo, Mkurugenzi Mtendaji wa UAP, Stephen Lokonyo alisema mchango huo ni sehemu ya utekelezaji wa sera ya uwajibikaji kwa jamii na umelenga kuhakikisha wanafunzi wanakuwa kwenye mazingira salama wakati wote wawapo shuleni na kupunguza hatari ya kupata magonjwa.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages