A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Monday, February 10, 2020

BARCLAYS BENKI TANZANIA SASA YAWA RASMI ABSA BENKI TANZANIA

01
Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT),Dkt Bernard  Kibesse (wa pili kushoto), na Mwenyekiti wa Bodi wa Benki ya Absa Tanzania, Simon Mponji (kulia), wakikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Benki ya Absa Tanzania ambayo awali ikiitwa Barclays Benki Tanzania. Wengine kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa  Wakala ya Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Emmanuel Kakwezi, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Abdi Mohamed na Mkurugenzi wa Chama cha wenye Mabenki (TBA), Tuse Jumbe. 
02
Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Absa Tanzania, Simon Mponji, akipokea cheti cha kubadilisha jina la kufanyia biashara kama  Benki ya Absa Tanzania kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Emmanuel Kakwezi (wa pili kushoto), katika hafla ya uzinduzi rasmi wa benki ya Absa Tanzania jijini Dar es Salaam jana. Awali iliitwa Benki ya Barclays Tanzania. Wanaoshuhudia kutoka  ni; Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Abdi Mohamed na Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, (BoT), Bernard Kibesse (wa pili kulia) pamoja na washuhudiaji wengine.
03
Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT),Dkt Bernard  Kibesse akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa Benki ya Absa Tanzania ambayo awali ikiitwa Barclays Benki Tanzania. Wengine kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi wa Benki ya Absa Tanzania, Simon Mponji, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Abdi Mohamed, Mkuu wa Kitengo cha Sheria na udhibiti wa Benki hiyo, Irene Sengati.
04
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Abdi Mohamed, akizungumza wakati wa  hafla ya uzinduzi rasmi wa Benki ya Absa Tanzania ambayo awali ikiitwa Barclays Benki Tanzania.
05
Wafanyakazi wa Benki ya Absa  Tanzania wakifanya maandamano ya amani kuashiria uzinduzi rasmi wa Benki ya Absa Tanzania ambayo awali ikiitwa Barclays Benki Tanzania.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages