A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Sunday, September 1, 2019

WATENDAJI KATA KUTUA DAR, RC MAKONDA AWAHAKIKISHIA KUWA HAKUNA WEZI'


MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, leo amewakaribisha   watendaji wa kata zote nchini  Katika Jiji la Dar es  Salaam, huku akiwahakikishia usalama wanapokuwa hapa tangu Septemba 2 mwaka huu kwa ajili ya mkutano uliondaliwa na Rais  John  Magufuli.

Rc Makonda ameyasema hayo alipofanya mkutano na wanahabari akielezea  kufurahishwa kwake na ujio huo  kuwa ni fursa kubwa kwa wafanyabiashara na wananchi wake ambapo mkutano huo utaongeza wigo wa biashara sehemu mbalimbali na kwamba hawatakumbana na kero za wezi katika jiji hilo.

"Ugeni huu katika mkoa wangu ni sehemu yake ya utaratibu ambao Rais wa awamu ya tano amejiwekea,ikiwemo kuzungumza na makundi mbali mbali ikiwemo viongozi wa dini  msishangae akawaita Wenyeviti wa serikali ya Mitaa ili ajue changamoto zao "alisema Makonda.


Amewataka wafanyabiashara kutumia nafasi hiyo kufanya biashara mbali mbali kwa dhumuni la kuutangaza mkoa wetu ambapo amewataka watendaji hao wanapofika Katika jiji Hilo waweze kutalii na kufurahia kufika Katika mko huo.

"Tukio la Rais kuwaita Watendaji Ni Jambo jema kwani anawapa  fursa watendaji kuwa Pamoja na kufahamishana Mambo mbalimbali Katika utendaji na hili si Jambo la kisiasa hivyo tuache kuingiza kazi na siasa watendaji ni watumishi wa Serikali anawaita kwa ajili ya kuwapa moyo"Amesema Makonda.


Wakati huohuo  Makonda amewataka wananchi kujenga tabia ya usafi kuanzia ngazi ya mtaa na kata,amewataka wenye nyumba barabarani kufunga taa Kila pande ili kusaidia  usalama Pamoja na kumfanya mtu kuwa na hofu ya kuchafua mazingira.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages