A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Wednesday, August 21, 2019

RC MAKONDA AMPONGEZA RAIS DKT. MAGUFULI KWA KUCHAGULIWA KUWA MWENYEKITI WA SADC

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda amempongeza Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Nchi 16 zinazounda Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika SADC ambapo amemtakia Utumishi mwema uliotukuka katika nafasi hiyo.

Aidha  amemshukuru Rais Magufuli kwa kuweza kupigania hoja ya Lugha ya Kiswahili kuingia katika Lugha Nne zinazotumiwa katika Jumuiya ya SADC na kuwahimiza Walimu, Baraza la Kiswahili Tanzania na wataalamu wa kiswahili kuchukulia hatua hiyo kama fursa ya ajira.

Hata hivyo amewataka Wafanyabiashara na wanachi kuchangamkia fursa za Kibiashara zinazopatikana katika nchi wanachama ikiwemo Fursa ya kuuza Vyakula na mazao.

Pamoja na hayo amewashukuru Wananchi wa Mkoa wa Dar es salaam kwa ukarimu na utulivu walioonyesha kwa kipindi chote cha Ugeni wa SADC jambo lililowezesha Wageni Kuingia nchini salama na kuondoka salama.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages