A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Thursday, August 8, 2019

NAIBU WAZIRI WA NISHATI AZINDUA MIRADI KUSAMBAZA UMEME PEMBEZONI MWA VIJIJI VYA CHALINZE NA BAGAMOYO


Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu, akizungumza wakati wa uzinduzi wa  Mradi wa Umeme Vijijini(REA), Katika Wilaya ya Bagamoyo na Chalinze Mkoni Pwani  ambapo mradi huo utafanywa na Mkandarasi kutoka Kampuni ya SINOTEC.

Mbunge wa Jimbo la bagamoyo Shukuru Kawambwa, akizungumza wakati wa uzinduzi wa  Mradi wa Umeme Vijijini(REA), Katika Wilaya ya Bagamoyo na Chalinze Mkoni Pwani  ambapo mradi huo utafanywa na Mkandarasi kutoka Kampuni ya SINOTEC
Baadhi ya viongozi waliohudhulia hafla ya uzinduzio huo 
Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu (wanne kushoto waliokaa), akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali pamoja na wafanya kazi wa Shirika la umeme Tanesco Bagamoyo.

Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu, akisalimiana na wakazi wa Chalinze waliohudhuria  ufunguzi huo
Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu (watatu kushoto waliokaa), akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali kulia kwa waziri ni Mbunge wa Jimbo la Chalize Ridhiwan Kikwete.
Mbunge wa Jimbo la Chalize Ridhiwan Kikwete (kulia), akisalimiana na Viongozi  kutoka Kampuni ya SINOTEC  wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu, ya uzinduzi wa  Mradi wa Umeme Vijijini(REA), Katika Wilaya ya Bagamoyo na Chalinze Mkoni Pwani  ambapo mradi huo utafanywa na Mkandarasi kutoka Kampuni ya SINOTEC.ya 

Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu, amewataka Meneja Tanesko kote nchini kuwa 
wabunifu  Katika kutatua changamoto za kukatika kwa umeme na  kuhakikisha umeme unakuwa wa uhakika.

Naibu Waziri wa Nishati ameyasema hayo Katika uzinduzi wa  Mradi wa Umeme Vijijini(REA), Katika Wilaya ya Bagamoyo na Chalinze Mkoni Pwani  ambapo mradi huo utafanywa na Mkandarasi kutoka Kampuni ya SINOTEC.

" Tunataka umeme unaosambazwa uwe wa uhakika kutokana na Juhudi za Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Magufuli za kupatikana kwa Nishati hasa vijijini naomba Sana Mameneja nchi nzima muwe wabunifu wa kutatua matatizo ya kukatika kwa umeme" Amesema Naibu Waziri.

Amesema Mradi huo utasaidia kupunguza changamoto za miradi ambapo umeme huu utawaka maeneo mbalimbali ikiwemo Shule, hospitali, sehemu za ujasiriamali Pamoja na makazi ya watu.

Aidha amewataka kampuni hiyo ya SINOTEC kuhakikisha wanafanya Kazi kwa wakati amabapo watafanya Kazi ndani ya miezi Tisa.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la bagamoyo Shukuru Kawambwa ameipongeza wizara ya Nishati kwa kuhakikisha Nishati inapatikana Katika Vijijini.

Amesema umeme huo utawasaidia wakazi wa Bagamoyo kupata umeme wa uhakika, na kuwataka kampuni iliyopewa dhamana ya kufanya Kazi hiyo kuifanya kikamilifu na kwa uhakika.

Fedha zilizotengwa kwa ajili ya kukamilisha Mradi wa Peri Urban Ni shilingi billion 12, na million 880.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa SINOTEC kwa ukanda wa Afrika Jin Hua, ameishukuru Serikali ya Awamu ya tano kwakuiami ni SINOTEC  na ameahidi kuwa anafanya kazi hiyo kwa  muda uliopangwa.

SINOTEC nikampini iliyofanya miradi kadhaa hapa nchini hivyo wanauzoefu mkubwa na imejiwekea uwaminifu  na historia nzuri  katika kazi walizofanya hapa nchini.

MATUKIO KATIKA PICHA










No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages