A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Tuesday, April 30, 2019

WHATSAPP KUTUMIKA KUWAHUDUMIA WATEJA WA TIGO

Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja wa Tigo Mwangaza Matotola, akiwaonyesha waandishi wa habari (hawapo pichani) namna ambavyo huduma ya WhatsApp inavyoweza kutumiwa na mteja kuuliza au kupata ufafanuzi kutoka kwa watoa huduma wa Tigo. Kushoto ni Meneja Mawasiliano wa Tigo Woinde Shisael.
Meneja Mawasiliano wa Tigo Woinde Shisael (kushoto) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa huduma ya WhatsApp ambayo inaweza kutumiwa na wateja wa kampuni hiyo kuuliza au kupata ufafanuzi wa bidhaa na huduma mbali mbali za kampuni hiyo. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja cha Tigo Mwangaza Matotola.
Kampuni ya Tigo Tanzania, imezindua huduma ya whatsApp kwa ajili ya kuwahudumia wateja wake. 

Huduma hii ya kidijitali, itawawezesha wateja wa Tigo kutuma dukuduku zao na kupokea majibu ya papo kwa papo watakapotumia namba ya WhatsApp ambayo ni 0675100100.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo mpya jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja wa Tigo Mwangaza Matotola alisema, Tigo imekuwa kampuni ya kwanza nchini kutumia mtandao wa kijamii wa WhatsApp kuwahudumia wateja wake. 

“Kupitia huduma hii mpya, wateja wa Tigo watapata uzoefu binafsi pamoja na kupata majibu ya papo kwa papo watapotaka kupata ufafanuzi wa jambo au utatuzi wa changamoto zozote katika kutuia mtandao wetu,” alisema

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages