Kampuni ya Tigo Tanzania, imezindua huduma ya whatsApp kwa ajili ya kuwahudumia wateja wake.
Huduma hii ya kidijitali, itawawezesha wateja wa Tigo kutuma dukuduku zao na kupokea majibu ya papo kwa papo watakapotumia namba ya WhatsApp ambayo ni 0675100100.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo mpya jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja wa Tigo Mwangaza Matotola alisema, Tigo imekuwa kampuni ya kwanza nchini kutumia mtandao wa kijamii wa WhatsApp kuwahudumia wateja wake.
“Kupitia huduma hii mpya, wateja wa Tigo watapata uzoefu binafsi pamoja na kupata majibu ya papo kwa papo watapotaka kupata ufafanuzi wa jambo au utatuzi wa changamoto zozote katika kutuia mtandao wetu,” alisema
No comments:
Post a Comment