A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Wednesday, April 17, 2019

TIGO YATOA ZAWADI ZA MAMILIONI KWA MAWAKALA WA TIGO PESA

Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa wa Tigo Pesa, James Sumari (kulia) akimkabidhi mfano wa hundi ya Sh. Milioni mbili, Mshindi wa Promosheni ya Mawakala wa Tigo Pesa iliyokuwa inajulikana kama ‘Cash In Promotion’, Said Khatibu kutoka Zanzibar, jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa wa Tigo Pesa, James Sumari (kulia) akimkabidhi mfano wa hundi ya Sh. Milioni mbili, Mshindi wa Promosheni ya Mawakala wa Tigo Pesa iliyokuwa inajulikana kama ‘Cash In Promotion’, Mojelwa Mlinga kutoka Dar es Salaam kwenye hafla iliyofanyika makao makuu ya Tigo, jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa wa Tigo Pesa, James Sumari (katikati) akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) muda mfupi kabla ya kukabiudhi zawadi kwa washindi wa Promosheni ya Mawakala wa Tigo Pesa iliyokuwa inajulikana kama ‘Cash In Promotion’,Kulia ni Mojelwa Mlinga, mshindi kutoka Dar es Salaam na kushoto Said Khatibu kutoka Zanzibar.
Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa wa Tigo Pesa, James Sumari (katikati) akiwapongeza kwa kuwanyanua mikono juu washindi wa Promosheni ya Mawakala wa Tigo Pesa iliyokuwa inajulikana kama ‘Cash In Promotion’. Kulia ni Mojelwa Mlinga kutoka Dar es Salaam na kushoto Said Khatibu kutoka Zanzibar.
Washindi wa Promosheni ya Mawakala wa Tigo Pesa iliyokuwa ikijulikana kama ‘Cash In Promotion’.Said Khatibu (kushoto) kutoka Zanzibar na Mojelwa Mlinga kutoka Dar es Salaam na (kulia) wakifurahia mfano wa hundi walizabidhiwa baada ya kuibuka washindi katika promosheni hiyo.
Kampuni ya Tigo Tanzania, jana imetoa zawadi za mamilioni ya shilingi kwa mawakala wake wa huduma ya Tigo Pesa kupitia promosheni iliyomalizika hivi karibuni ya ‘Wakala Cash In Promotion’.

Promosheni hiyo ya nchi nzima ilianza Machi 1 na kumalizika Machi 31 ikilenga kuwahamasisha mawakala wa Tigo Pesa kufanya miamala zaidi na wateja ili kujishindia zawadi za fedha taslimu.

Akizungumza wakati wa kutoa zawadi kwa baadhi ya washindi jijijni Dar es Salaam jana,mkuu wa kitengo cha bidhaa wa Tigo Pesa James Sumari alisema jumla ya Mawakala 97,000 walishiriki katika promosheni hiyo ya mwezi mmoja.

“Promosheni hii ya aina yake, ni ya saba kwa Mawakala wetu. Tangu tulipoanza hadi kufikia hivi sasa, tumewazawadia mawakala 12,000 zaidi ya fedha taslimu shilingi bilioni 1. Washindi hawa wametoka kila kanda hapa nchini na tumeendelea kuona mwitikio mkubwa wa Mawakala kupitia promosheni hii na ni mpango wetu kuendelea kuwarushia tunachokipata kupitia wao wakati tukiendela na safari ya kufikisha huduma jumuifu za kifedha nchi nzima,” alisema Sumari

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages