Mamlaka nchini Uganda zimesema watu 18 wamethibitishwa kufariki na wengine 100 kujeruhiwa baada ya mvua kubwa kunyesha na kusababisha mafuriko wakati wa usiku kwenye Wilaya mbili Mashariki mwa Uganda.
Msemaji wa Polisi wa eneo la Busoga, Michael Kasadha alisema kuwa watu 13 walifariki kwenye wilaya ya Buyende na wengine 5 katika Wilaya ya Kamuli usiku wa Jumatatu.
Maeneo yaliyoathiriwa vibaya na mvua hiyo yako kwenye uwanda wa chini karibu na mto Kyoga.
No comments:
Post a Comment