A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Sunday, February 10, 2019

SmartLab yafanya mkutano wa 3 wa wavumbuzi uitwao Mwanzilishi kwa Waanzilishi




Baadhi ya washiriki wa jukwaa la Founder 2 Founder iliyoandliwa na SmartLab wakifurahia kupata selfi ya kumbukumbu baada ya kongamano kuisha



SmartLab yafanya mkutano wa 3 wa wavumbuzi uitwao Mwanzilishi kwa Waanzilishi

Smartlab leo imefanya awamu ya tatu ya mfululizo wao wa Mwanzilishi kwa Waanzilishi katika ofisi za Seedspace, Victoria, Dar es Salaam Tanzania kualamisha mwanzo wa matukio yao waliyopanga kwa mwaka 2019.
Smartlab imekua ikileta pamoja watu wa umuhimu kwenye sekta ya uvumbuzi kwa jioni za maongezi na kufundishana miongoni mwa hao waanzilishi. Wanafanya hivyo kupitia majadiliano kwenye mada tofauti tofauti ili kupata ufahamu wa jinsi ya kukuza kampuni mpya. Tukio lilikua na mandhari ya “Jinsi ya kukuza kiufanisi soko la kampuni yako mpya” na ilikua na jopo la watu kutoka sekta tofauti.
Mwanzilishi kwa Waanzilishi ni jukwa kwa ajili ya kampuni mpya kukutana na wawekezaji, waanzilishi wenza na washirika. Na inawawezesha kuungana na kushirikiana wakati wanbadilishana mawazo ya ubunifu kwa ajili ya kukua, kubadilisha mitazamo na kutengeneza ufumbuzi wa kubadilisha mazingira ya Tanzania na Africa kwa ujumla.
Akiongea kwenye tukio, Edwin Bruno, Mwanzilishi wa SmartLab na mkurugenzi mtendaji wa Smart codes Limited alisema kwamba “Kampuni mpya, wajasiriamali, wabunifu na wavumbuzi wa biashara za hapa nyumbani sasa wana sehemu moja ya kukutana na kufanya shuguli ambazo zitakutanisha na kukuza jumuiya za uvumbuzi zilizo tofauti na zenye vipaji hapa Tanzania na africa kwa ujumla kupitia Mwanzilishi kwa Waanzilishi”, Pia alieleza kua “Jukwaa la Mwanzilishi kwa Waanzilishi linatoa muungano wa muhimu ambao unawezesha wajasiriamali na kampuni mpya kujua mienendo mipya kwenye sekta ya uvumbuzi. Pia inawapa uwezo wa kujielezea kuhusu changamoto zao na hivyo kutengeneza nafasi za suluhisho kwa ajili ya mapungufu yao”.

Bwana Kumeil Abdulrasul, Bidhaa na ushirikiano, Raha Liquid Telecom, mdhamini mkuu wa tukio aliongeza “Tunajivunia kua sehemu ya tukio la SmartLab Mwanzilishi kwa Waanzilishi awamu ya tatu. Ubunifu ndio hatima ya miaka ya mbele na Raha Liquid Telecom inajivunia kua sehemu ya timu ambayo inataka kubadili hatima ya ubunifu, kampuni mpya na mazingira ya ubunifu Tanzania”.

Smart Lab ni jukwaa la ubunifu linalo unganisha taasisi za elimu na mashirika suluhisho mapya ambayo zitaleta athari nzuri katika jumuiya za Africa.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages