A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Thursday, February 28, 2019

Elimu Inatakiwa kupunguza Utapiamlo

DSCN0157-min
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Mradi wa Lishe Endelevu  baada ya kikao kilichofanyika katika Hoteli ya Nashera Mjini Morogoro. Kutoka kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Malinyi Mhe. Majura Kasika, Meya wa Manispaa ya Morogoro Mhe. Pascal Kihanga, Mratibu wa Mradi wa Lishe Endelevu Dkt. Joyce Kaganda na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Frank Jacob
…………………….
Na Andrew Chimesela – Morogoro.

Imeelezwa  kuwa tatizo sugu la utapia mlo unaendelea kuwa tatizo hapa nchini kwa baadhi ya maeneo unatokana na ukosefu wa Elimu inayopelekea watu wengi kuwa na utamaduni wa kula vyakula vyenye viinilishe vya aina moja badala ya kula vyakula vyenye mlinganyo  wa virutubishi.
Kauli hiyo imetolewa Mwanzoni mwa wiki hii na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe wakati wa ufunguzi wa Kikao cha kutambulisha Mradi wa Lishe Endelevu kilichofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Nashela iliyopo Manispaa ya Morogoro.

Dkt. Kebwe amesema watu wengi wanapata chakula cha kutosha laikini kinachokosekana ni kukosa  kula chenye Chakula chenye mchanganyiko wa virutubishi vyote muhimu ukiwemo Mkoa wa Morogoro ambao hauna tatizo la chakula ila watu kutokula vyakula vyenye mlinganyo wa virutubishi.

“Kwa Mkoa wa morogoro chakula sio tatizo, tatizo ni kutokula vyakula vyenye mlinganyo unaotokana na kukosa wa Elimu”.Alisema Dkt. Kebwe.
Amesema Morogoro unachangia akiba ya chakula hapa nchini kwa asilimia 30 na mchele wote unaoliwa na watanzania asilimia 52 ya mchele huo unatoka Mkoa wa Morogoro, hivyo  amesisitiza kuwa Morogoro chakula sio tatizo, tatizo ni kutokuwa na uelewa wa kula vyakula vyenye mlinganyo hivyo aameshauri Mradi wa Lishe endelevu kutoa Elimu hiyo kwa nguvu zote.

Naye Mratibu wa Mradi wa Lishe Endelevu unaofadhiriwa na Watu wa Marekani kupitia Shirika la Save the Chidren  Dkt. Joyce Kaganda amesema takwimu za utapiamlo kitaifa zinaonesha unapungua kwani 2010 kulikuwa na asilimia 42 ya utapia mlo, kwa sasa ni asilimia 34 na mpango wa Taifa wa maendeleo umedhamiria kupunguza utapia mlo hadi kufikia asilimia 28.

Hata hivyo Dkt. Kaganda amesema Mradi wa lishe endelevu kwa sasa utajikita katika kuhamasisha masuala ya uratibu wa shughuli za Lishe Endelevu hapa nchini  pamoja na kuweka mipango ya kuongeza Bajeti ya utekelezaji wa shughuli za Lishe Endelevu ikiwa ni pamoja na kutoa Elimu ya watu kubadili tabia kula vyakula vyenye virutubishi vyote.

Kwa upande wa wajumbe walioshiriki kikao hicho wakiwemo Wakuu wa Wilaya, na Wakurungenzi wa Halmashauri huku Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Siriel Mchembe alisema ili kuweza kufikia malengo ya mwaka 2020/2021 kuna haja ya wananchi kutumia vema fursa ya maeneo yao kulima mazao yenye virutubishi vingi likiwemo zao la viazi.

Huku Mkuu wa Wilaya ya Malinyi Mhe. Majura amesema ili kujenga kizazi bora na chenye Afya ni vema Elimu ikatolewa kwa jamii kuhusu malezi yanayotakiwa na vyakula vinavyotakiwa kuliwa na mama Mjamzito tangu kutungwa mimba kwa mtoto, kulelewa hadi kufikia siku elfu moja ambazo ni muhimu kwa mtoto.

Mradi wa Lishe Endelevu unaofadhiriwa na USAID kupitia Shirika la Save The Chidren ni mradi wa miaka minne utakaotekelezwa kwa mikoa minne hapa nchini ambapo kwa Mkoa wa Morogoro utatekelezwa kwa Halmashauri zote tisa za Mkoa huo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages