A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Friday, May 11, 2018

Vanessa Mdee akutana na producer wa Michael Jackson na Celine Dion


Vanessa Mdee amekuwa akipambana kwa kila hali kuhakikisha muziki wake unafika mbali zaidi. Msanii huyo amekutana na producer na audio engineer, Humberto Gatica ambaye ni mshindi wa tuzo 16 za Grammy na kufanya naye kazi.

Vanessa amekutana na producer huyo katika studio maarufu duniani ya Abbey Road iliyopo nchini Uingereza na kutengeneza project ya kazi kwa ajili ya tamasha la Bantu Jazz litakalofanyika Juni 9 ya mwaka huu nchini Garbon.


Akiongea na mtangazaji Fredrick Bundala, Vee Money amesema kuwa Gatica pia atakuwepo kwenye tamasha hilo litakalofanyika Garbon.

Gatica amewahi kufanya kazi na wasanii wakubwa duniani akiwemo Barbra Streisand, Mariah Carey lakini kubwa zaidi ni Thriller ya Michael Jackson, My Heart Will Go On ya Celine Dion na nyingine.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages