Baada ya kuripotiwa kuwa nyota wa zamani wa Manchester United na timu ya
taifa ya England Wayne Rooney kuwa anaondoka kwenye klabu ya Everton
mwisho wa msimu huu, imeelezwa kuwa ni kutokana na ugomvi na kocha Sam
Allardyce.
Magazeti ya michezo nchini England, leo yameripoti kuwa Rooney
ameishinikiza Everton kumwondoa kocha Sam na kama hawatafanya hivyo basi
yeye ataondoka ili kumpisha kocha huyo ambaye.
Rooney alirejea Everton msimu huu akitokea Manchester United ambako
alicheza kwa mafanikio kutoka mwaka 2004 hadi 2017. Ikumbukwe kuwa
Everton ndio sehemu aliyoanzia maisha ya soka kabla ya kutua Man United.
Wakala wa Rooney yupo nchini Marekani kumalizia hatua za mwisho
kukamilisha uhamisho huo wa mkongwe huyo kuelekea katika klabu ya DC
United inayoshiriki ligi kuu ya Marekani (MLS).
Kwa upande wake kocha wa Manchester United Jose Mourinho aliyemfundisha
Rooney kwa msimu mmoja amesema maisha ya soka ya Rooney ndani ya England
yameenda vizuri hivyo ni haki yake kubadili uelekeo.
Post Top Ad
Your Ad Spot
Friday, May 11, 2018
Kuondoka kwa Rooney Siri yafichuka
Tags
MICHEZO#
Share This
About kilole mzee
MICHEZO
Labels:
MICHEZO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Your Ad Spot
No comments:
Post a Comment