Msanii wa BongoFleva na mjasiliamali nchini Tanzania, Zuwena Mohamedy
maarufu kama 'Shishi Babe' amefunguka na kuwataka baadhi ya wanaume
wenye tabia ya kuvaliana au kuazima nguo hasa za ndani kuacha mara moja
kwa kuwa jambo hilo sio zuri.
Shishi Babe ametoa kauli hiyo siku za hivi karibuni wakati alipokuwa
anazungumza kwenye kipindi cha DADAZ kinachorushwa na tinga namba moja
kwa vijana EATV kila siku ya Jumatano kuanzia saa 5:00 asubuhi hadi 6:00
mchana baada ya kuulizwa swali na waongozaji wa kipindi hicho kuwa ni
kwa nini watu wanapenda kuazima vitu na kushindwa kurudisha.
"Zamani wanawake walikuwa wanaongoza kwa kuazimana lakini hivi sasa
mpaka wanaume wanaazimana nguo mpaka za ndani. Mimi sipendi kabisa
masuala ya kuazimana vitu haswa nguo kama wanavyofanya wadada wengine wa
mjini na kama mtu akija kuniazima kitu kwangu huwa naangalia na muda
mwingine naigawa kabisa na siwezi kuichukua tena", amesema Shishi Babe.
Post Top Ad
Your Ad Spot
Friday, May 11, 2018
Shilole awafungukia wanaume wanaoazima nguo
Tags
FILAMU#
Share This
About kilole mzee
FILAMU
Labels:
FILAMU
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Your Ad Spot
No comments:
Post a Comment